0
 
Wakati mchakato huo ukisubiri mashabiki kuamua msanii yupi aingie katika kipengele kipi, wasanii wengi watakuwa matumbo joto kwa kile kinachoelezwa kwamba KTMA sasa zimekubalika zaidi kwao na mashabiki wa muziki.

Msimu wa utoaji tuzo kwa wasanii wa muziki Tanzania wanaofanya vizuri umewadia huku mchakato wa awali wa mchanganuo wa tuzo hizo za Kili Tanzania Music Awards 2015 (KTMA) ukianza rasmi wiki hii.
Wakati mchakato huo ukisubiri mashabiki kuamua msanii yupi aingie katika kipengele kipi, wasanii wengi watakuwa matumbo joto kwa kile kinachoelezwa kwamba KTMA sasa zimekubalika zaidi kwao na mashabiki wa muziki.
Hata hivyo, msimu huo unatojawa kuwa wenye neema kwa wasanii, unazua maswali mengi vichwani mwa wasanii na mashabiki wao moja likiwa; ni nani atavunja rekodi iliyowekwa na mwanamuziki Diamond Platnumz mwaka jana?
Mbali na Diamond kuvunja rekodi msimu uliopita, Bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa pia iliwahi kunyakua tuzo tano mwaka 2013, huku wasanii, Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz wakinyakua tuzo tatu kila mmoja.

Post a Comment

 
Top