Meneja Mradi wa Kamati ya Uangalizi wa Chaguzi Tanzania (TEMCO), Dk Benson Bana,
Dar es Salaam. Zaidi ya Sh720 bilioni
zitatumika kuanika ‘uozo’ wakati wa mchakato wa uandikishaji wapiga
kura, kura ya maoni na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Akitoa taarifa hiyo jijini Dar es Salaam jana,
Meneja Mradi wa Kamati ya Uangalizi wa Chaguzi Tanzania (TEMCO), Dk
Benson Bana, alisema kuwa fedha hizo zimetolewa na Shirika la Misaada la
Marekani (USAID) kuwezesha mpango huo kufanikiwa.
Alisema kuwa kwa mara ya kwanza kamati hiyo, pia
itaangalia mchakato wa uteuzi wa wagombea ndani ya vyama vya siasa,
utakaojumuisha wagombea urais, ubunge, ujumbe wa Baraza la Wawakilishi
na Udiwani.
Baada ya kumalizika kwa hatua hiyo, TEMCO
itaandika ripoti ikatakayoweka wazi mbinu mbalimbali zinazotumiwa na
wanasiasa kuteua na kushinda nafasi wanazogombea ikiwamo kununua kura.
“Watazamaji wa uchaguzi watakuwa makini kuangalia
mifumo ya kisheria na kitaasisi, uteuzi wa wagombea ndani ya vyama vya
siasa, uthabiti wa tume za uchaguzi, utekelezaji wa Sheria ya gharama za
Uchaguzi na uteuzi wa wagombea unafanywa na tume za uchaguzi,” alisema
Dk Bana.
Aliongeza: “Tunafuatilia ili wananchi wa kawaida
wawe na imani na mfumo wa uchaguzi katika nchi yao. Uchaguzi wa mwaka
2000 watu wengine walikuwa wanaogopa kusema sisi tulitokea tukasema
hakukuwa na uchaguzi bali uchafuzi na tulifikiri wangetufukuza
hawakufanya hivyo.”
Vile vile, TEMCO itaangalia upigaji kampeni,
masuala ya jinsia, utendaji wa vyombo vya habari na matukio
yatakayojitokeza wakati wa kupiga kura ikiwamo kuhesabu kura, kukusanya
na kutangaza matokeo.
Dk Bana alisema zoezi hilo lililofadhiliwa na
Shirika la Misaada la Marekani (USAID), litasimamiwa na watazamaji wa
muda mrefu 180 watakao angalia zoezi la uandikishaji wapiga kura
litakaloanza Februari mwaka huu.
Watazamaji wa muda mfupi 6,400 wanatarajiwa
kuangalia shughuli za kila siku ya kupiga kura ya maoni, Uchaguzi Mkuu
utaangaliwa na watazamaji wa muda mrefu 118 na 7,000 wa muda mfupi
watakaopangwa katika vituo mbalimbali Tanzania Bara na Zanzibar.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Bara, John Mnyika
uamuzi huo ni mzuri lakini wamechelewa kwa sababu hawapaswi kusubiri
mpaka wakati wa uchaguzi wa ndani walitakiwa kuanza sasa wakati wa zoezi
la kuandikisha wapiga kura.
“Haipaswi kuwa TEMCO pekee, waangalizi wa ndani
wanapaswa kuwa wa kamati na taasisi mbalimbali ili kuwe na ulinganishi
isije ikawa kamati moja inatumika vibaya,” alisema Mnyika.source:mwananchi
Post a Comment