Kuna utata juu ya Kasri ya Nkandla iliyopo kilomita 24 kutoka mjini Nkandla, Kwa Zulu-Natal ina milikiwa na raisi wa Afrika Kusini mheshimiwa Jacob Zuma. Inasemekana pesa zilizotumika kujenga eneo hili ni za uma. Utata huu ulisababisha vurugu katika bunge la nchi hiyo alipokua akihutubia wabunge wiki hii. Wabunge wa upinzani walihoji bila kufuata utaratibu wa bunge ni lini atarudisha pesa za uma alizotumia kwa maslahi yake binafsi?. Utata wa hali hii umepewa jina=>Nkandlagate
.
Bunge la Afrika kusini liligeuka
kuwa uwanja wa vita ambapo wabunge wa upinzani ilifikia hatua ya
kuvutana mashati na maafisa wa usalama na kufanya wabunge wa upinzani wa
chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) wakiongozwa na Julias Malema
kutolewa nje ya ukumbi wa bunge kwa nguvu na baadae wabunge wengine wa
upanzani nao wakatoka nje ya ukumbi.
Sakata hilo lilizuka wakati
Rais wa nchi hio Jacob Zuma alipokuwa akilihutubia taifa na kuulizwa
maswali na wabunge wa chama cha EFF kinachoongozwa na Julius Malema
wakitaka kujua ni lini atarejesha pesa zilizojengea jumba lake la
kifahari la NkandlaHayo yanatokea wakati kuna baadhi ya maeneo nchini humo wanaishi katika mazingira haya(pichani)
How the other half live: The spending sparked
public anger amid an economic crunch in a country where 10 million
people live on social grants and many have only tin shacks for their
homes
Post a Comment