Kampuni
kubwa ya uzalishaji wa mafuta Duniani ya Schlumberger imesema
itapunguza ajira kwa kiwango cha asilimia saba kutokana na kuanguka kwa
bei ya mafuta ulimwenguni.
Hatua hiyo ya kupunguza
wafanyakazi inakuja kufuatia hali iliyotarajiwa ikiwemo matarajio kidogo
ya tofauti na gharama ya ugunduzi na uzalishaji wa mafuta kwa mwaka
2015. Makampuni tanzu ya mafuta ya Schlumberger yamepunguza ghrama za
uchimbaji mafuta kutokana na anguko hilo la bei. Bei ya mafuta katika
soko la Dunia imeanguka kwa zaidi ya asilimia 50 tangu mwezi June
mwakajana hali inayoathiri mataifa ambayo yamekuwa yakinufaika na
biashara za mafuta Duniani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment