0
MWAANDISHI WETU Nachingwea
,Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi uliofanyika  kimefanikiwa kushinda vijiji 100 sawa na asilimia 80.64 kati ya vijiji 124 vilivyofanya uchaguzi  huo ambao kwa baadhi ya maeneo yaligubika na vurugu ambapo vijiji vitatu havikufanya uchaguzi.
Kwa mujibu wa msimamizi wa uchaguzi wa halmashauri ya wilaya ya Nachingwea,Boniface Chatila,alisema kuwa  Chadema  imenyakuwa  vijiji 12 sawa na asilimia 9.68 ,Cuf imeweza kupata vijiji 12 sawa na  asilimia 9.68.
Kwa upande wa  vitongoji Msimamizi huyo alisema kuwa CCM imeshinda vitongoji 405  sawa na asilimia 79.72 kati ya vitongoji 526 ambapo vitongoji 18 havikufanya uchaguzi huo,Chadema imeshinda vitongoji 51 sawa  na  asilimia 10.04 Cuf imeshinda vitongoji 51 sawa na asilimia 10.04 na ADC ikiambulia kitongoji kimoja sawa na asilimia 0.2.
Chatila alitaja sababu ya  vijiji na vitongoji hivyo  kutofanya uchaguzi  kuwa ni pamoja kukosekana kwa karatasi za kupigia kura,makosa ya uchapaji kwenye karatasi za kupigia kura na kuwa vijiji  na vitongoji hivyo vinaendelea kufanya uchaguzi huo  na kuwa hadi kufikia mwishoni mwa wiki hii maeneo yote yatakuwa  yameshafanya uchaguzi.
“Maeneo yasiyofanya uchaguzi ilitokana na makosa ya uchapaji  kwani baadhi yalichanganya majina ya wagombea “alisema Chatila.
Akizungumzia  juu ya uchaguzi huo mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Nachingwea.

Post a Comment

 
Top