Taarifa
kutoka Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zinasema kuwa wanamgambo wa Boko
Haram wamefanya shambulizi lengine kubwa sana na kuwaua takriban wafanya
biashara 50 wa kuuza Samaki katika ufuo wa ziwa Chad.
Shambulio
hilo lilifanyika Alhamisi lakini kutokana na matatizo ya kimitambo,
taarifa za mauaji hayo hazikuweza kutolewa punde yalipofanyika.
Siku moja
kabla ya mauaji hayo, zaidi ya watu arobaini waliuwa na wanamgambo hao,
katika shambulizi lililofanya peupe mchana katika jimbo la Borno.
Wafanyabiashara hao, walikuwa njiani kununua Samaki waliposhambuliwa na wapiganaji wa Boko Haram.
Boko Haram
waliziba barabara karibu na kijiji cha Doron Baga na kulingana na
kiongozi mkuu wa shirika la wafanyakazi hao wakawachinja wengi wa
waathiriwa wengine wakifungwa kamba na kuzamishwa majini katika ziwa
Chad.
Nia ya shambulizi lao haikujulikana mara moja.
Eneo
lililoshambuliwa linapaswa kuwa na kikosi cha wanajeshi kinachoshika
doria, lakini kikosi cha wanajeshi hao kutoka Nigeria , Chad na Niger
hakijaweza kudhibiti hali katika eneo lenyewe kama ilivyotarajiwa kwani
wameshindwa kulikomesha kundi la Boko Haram kufanya mashambulizi ya mara
kwa mara.
Hili lilikuwa shambulizi la pili kubwa kufanyika katika jimbo la Borno wiki jana na kwa jumla takriban watu 100 waliuawa.
Mnamo siku
ya Jumatano, wapiganaji hao walivamia soko moja katika eneo la Aazara
Kuya. Watu 45 walikamatwa huku wakifungwa mikono na kukatwa koo zao.
Shambulizi hili inaarifiwa lililengwa kuadhibu jamii baada ya wanamgambo wanne kutambulishwa kwa wanajeshi na kuuawa.
Chanzo - BBC Swahili
Post a Comment