Mchezaji wa siku nyingi nchini Brazil na
aliyeiwezesha Brazil kunyakua kombe la Dunua mara tatu amelazwa
hospitali ya mjini Sao Paulo kwa maambukizi baada ya kufanyiwa upasuaji
kuondoa mawe kwenye figo ya mchezaji huyo.
Pele mwenye miaka 74 alilazwa kwenye
hospitali hiyo jumanne wiki hii baada ya kupata maambukizi kutokana na
kufanyiwa upasuaji kuondoa mawe kwenye figo mwezi uliopita.
Madaktari wa hospitali ya Albert Einstein
ya mjini Sao Paulo wamesema hali ya mchezaji huyo inaendelea kuimarika
lakini habari kutoka kwa shirika la habari la AFP zinasema hali ya
mchezaji huyo inaendelea kuwa mbaya amewekwa chini ya uangalizi maalum
kwenye chumba cha wagonjwa mahututi.
Post a Comment