0


WAFUGAJI WAINGIA ndani ya msitu wa hifadhi Nyera Kipelele wilayani Liwale mkoani Lindi kuendesha malisho



MBUNGE APORA ARDHI YA WANANCHI.
Na mwaandishi wet liwale.
Liwale.Wananchi wa Kijiji cha Kibutuka wilaya ya Liwale,mkoa wa Lindi wanalalamikia kitendo cha Mbunge wao,Faith Mohamed Mtambo kumilikishwa  eneo lenye madini aina ya Manganise bila kufuata taratibu zilizoainishwa na sheria ya ardhi namba 5,1999 na sheria ya Madini ya mwaka 2010 pamoja na Sera zake hivyo kusababisha mgogoro kati ya wanakijiji na mbunge huyo.
Akizungumzia Mgogoro huo, mkazi wa kijiji cha Kibutuka, Chande Majate alisema  wananchi wa kijiji hicho wamestushwa na kitendo  cha Mbunge huyo kumilikishwa eneo hilo tangu mwaka 2011 bila wao kushirikishwa, na kuwa   hawajui ametumia taratibu gani za kisheria kumiliki eneo  ambalo wamiliki halali na serikali ya kijiji.
Alisema kuwa eneo hilo ambalo iwapo litachimbwa kwa kutumia mitambo ya kisasa linaweza kufanya kazi kwa muda wa zaidi ya miaka ishirini na tano lina  madini ya aina ya Manganise ambayo yanatumika kama urembo  majumbani na pia kuna aina nyingine saba za madini ikiwemo dhahabu, shaba na mengine.
Alibainisha kuwa eneo hilo liligunduliwa na wenzao wawili wa kijiji hicho, Abdul Kujakila na Hemedi Majate  baada ya kuyaona mawe ndipo waliyachukua na kumtafuta mtu mwenye  uzoefu na masuala ya madini  ambaye aliwajulisha kuwa mawe hayo ambayo pia  yameenea katika maeneo mengi kwenye kijiji hicho  na vijiji jirani ni madini ya manganise.

Alisema kuwa baada ya ugunduzi huo serikali ya kijiji  baada kupata baraka ya mkutano wa kijiji ilimpa kibali Faridi Mpili ili aanze  mchakato wa kupata hati miliki ya  eneo hilo ambalo lina ukubwa wa kilometa za mraba 70 ili kuanza uchimbaji kwa sharti la kuingia ubia na wananchi wa kijiji hicho wa kushirikisha wachimbaji wadogo wadogo.
 Kwa upande wake,Ramadhani Kwepu,Mkazi wa kijiji cha Kibutuka alionesha kushangazwa na mchakato mzima wa kumpatia hati mbunge huyo kwani katika mchakato huo wananchi ambao ndio wenye mamlaka ya kuridhia upatikanaji wa ardhi ya kijiji hicho hwakushirikishwa  hali inayotia shaka kwa uwepo mazingira ya rushwa .
Alisema kuwa walishangaa  kuwaona watu waliojiita wawekezaji ambaye ni  Francis Mutalemwa na wenzake kwenye  eneo hilo ambalo licha ya kuwa katika kijiji cha Kibutuka linajumuisha na vijiji vya jirani ambavyo hata  uongozi wa vijiji vyao hauna taarifa  ya  maeneo yao kumilikiwa na Mbunge huyo ambao walianza kuchimba bila ya kufuata taratibu na kudai kuwa wao walitumwa na Faith Mtambo jambo lilisababisha wananchi kuwatimua huku wakitelekeza madini yenye uzito unaokadiriwa kuwa Tani mia tano,
Kwepu ambaye ni mmoja kati ya wajumbe wanaofuatilia sakata hilo la umiliki wa Kampuni iliyotambulika kwa jina la Linda Ruta company ambayo imebainika ni jina la mmoja wa Mtoto wa Mbunge huyo, alibainisha kuwa licha ya kudai eneo hilo ambalo  pia linagusa maeneo ya vijiji vya Kiangara,Mihumo,Nangano,Kipelele,Ngumbu na Kitogoro kumilikiwa na Mtoto wa mbunge huyo, anayetoa maelezo na kutajwa ni Mbunge Mtambo badala ya Linda ambaye inadaiwa kuwa ndiye anamiliki.
  Alisema kuwa kutokana na uwepo wa mgogoro huo  kuna mawe yenye uzito wa Tani zipatazo 500 za madini ya manganasi yanashindwa kuondolewa ambayo yalivunjwa na Mutalemwa na wenzake kufuatia kutimuliwa na kusitishwa na uongozi wa kijiji kwa kushirikiana na wananchi.
Hamisi Kichoti mkazi wa kijiji cha Kibutuka  Alishangazwa na kauli ya Mbunge huyo kuwa anawafahamu na kuwa atawataja wamiliki  wengine wa vitalo vingine kati ya vitalu 12 vilivyopo katika eneo hilo  lakini hajawataja wamiliki hao hali inayotia shaka  kuwa uenda hata  vitalu  vingine vinamikiwa  na mbunge huyo.
"Kitendo cha Mbunge huyo kusema kuwa anawajua wamiliki wa vitalu vingine inatia shaka kuwa uenda vitalu vyote vinavimilikiwa yeye"alibainisha Kichoti.
Alisema  mbunge huyo kama kweli anataka kumiliki eneo hilo afuate tararatibu za kisheria kwa kupeleka maombi kwa serikali ya kijiji ambapo ataeleza wananchi wapatao 7,890 wanaoishi kwenye maeneo hayo watakavyopata  fidia kutokana na eneo lao kumikiwa, ambapo vijiji husika vitanufaika na nini kwa uwepo wa mgodi huo.
   Mwenyekiti wa kijiji hicho, Rajabu Kwepu alikiri kuwa upo mgogoro huo ambao alisema kuwa licha ya mbunge huyo kukiri na kuomba radhi kupitia mkutano mkuu wa kijiji kuwa anamiliki bila kushirikisha wananchi na kuwa angekuja rasmi kufafanua hoja hiyo lakini hajafika kijijini hapo.
Aidha alibainisha kuwa wananchi  walimtaka awataje wamiliki wengine wa vitalu ambapo mbunge huyo alidai anawafahamu na kuwa atawataja jambo ambalo hajalitekeleza hadi hivi sasa na hivyo ametakiwa  kutekeleza makubaliano hayo.
"Tulimwita kwenye mkutano wa wananchi wote  uliofanyika mwezi wa tatu mwaka huu u ili awataje wamiliki wa vitalu vingine kama alivyoahidi hata hivyo hajalitekeleza ahadi hiyo"alisema Kwepu.
Mwenyekiti wa kijiji cha Mikunya,Saidi Mkongoteka,moja ya kijiji ambacho limo eneo ambalo linamilikiwa alisema uongozi wake umepata taarifa zisizo rasmi juu ya Mbunge kumiliki eneo kubwa ambalo kijiji chake kimo ndani ya eneo hilo na kuwa  kwa sasa wanafuatilia kuona ukweli wa  jambo hilo.
Alibainisha kuwa iwapo ikibainika kuwa taarifa hizo ni za kweli Serikali ya kijiji hicho haitakubalia hivyo kumtaka mbunge huyo kuacha kabisa eneo hilo na kuwa uenda ikachukua hatua za kisheria za kisitisha umiliki huo.
"Kwa sasa tunafuatilia ukweli wa taarifa hii kwa hatujaipata rasmi,hata hivyo namtaka ndugu yangu(Mbunge) kuachana na eneo hili kwa tukibaini kuwa zinaukweli hatutasita kumfikisha kwenye vyombo vya sheria ili kusitisha umiliki wake"alisema Mkongoteka.
Naye, Nasoro Pyandu mjumbe wa serikali ya kijiji cha Kitogoro ambacho nacho kimekumbwa kwa eneo lake kuwa ndani ya eneo la mbunge huyo, alieleza kuwa hawajapokea  ombi lolote la kampuni au mwekezaji la kutaka umilikiwa wa eneo hilo kwa lengo la kuchimba au kufanya utafiti wa Madini na kuwa anayo taarifa ambazo si rasmi kuwa Mbunge anamiliki eneo kubwa ambalo limeingia hadi kwenye kijiji chao.
Alisema kuwa iwapo jambo hilo litakuwa na ukweli basi anaomba uongozi wa kijiji hicho kuitisha mkutano wa kijiji ili ujadili kwa kina na  kupata ufumbuzi na  uamuzi wa pamoja  kwani eneo hilo ni mali ya wananchi wa kijiji hicho kisheria.
“Lisemwalo uenda lipo hivyo Iwapo kuna ukweli au la juu ya umiliki huo, nadhani busara ambayo nitawaomba viongozi wetu ni kuitisha mkutano wa wananchi wote ili watoe uamuzi juu ya ardhi yao"alisema Pyandu.
Faridi Mpili ambaye awali aliwabainishia wananchi hao kuwa mawe yaliyopo kwenye kijiji hicho ni madini ya Manganise alisema baada ya kugundua kuwa eneo hilo lina madini hayo uongozi na wananchi kupitia mkutano wa kijiji walimpa kibali cha kuanza mchakato wa kupata hatimiliki na kuwa baada ya kuwasilisha barua hizo ofisi ya Madini kanda ya kusini akakuta eneo hilo linamikiwa na Mbunge,Faith Mtambo tangu 28/12/2011 akitumia kampuni iliyotambukika kwa jina la Linda Ruta company.  
 Kwa upande  wake,Mkuu wa wilaya ya Liwale,Hephrem Mmbaga alikiri kuwepo kwa mgogoro huo baada ya suala hilo kufikishwa mahamakani na Francis Mutalemwa  na wenzake ambao walipinga kusimamishwa shughuli za uchimbaji ambapo mkuu huyo alisema ofisi yake haina mamlaka ya kuingilia masuala ya madini na kuwa uwezo wake ni kuhakikisha hakuna migogoro kwa kutoa ushauri kwa Kamishna wa Madini.
"Jukumu langu mimi  kama Mkuu wa wilaya ni kutoa ushauri kwa kamishna wa madini iwapo kunajitokeza stofahamu ... kwani hata wanapofanya shughuli zao sheria haiwalazimishi kutoa taarifa kwangu na hii sisi kama wakuu wa wilaya tumekuwa tukiipinga sana na kutaka hii shreia iangaliwe upya"alisema Mmbaga.
 
Kamishna wa  Madini kanda ya Kusini inazungumziaje.
Kamishna wa madini kanda ya Kusini, Injinia Benjamini Mchwampaka, alisema  kuwa hana taarifa ya mgogoro huo kwa kuwa ni mgeni hivyo alisema ataitahitaji muda ili kuangalia kumbukumbu  za ofisi kuona  undani wake.  
"Binafsi mimi hapa ni mgeni kabisa ila ninachojua ni kuwa ofisi inatoa leseni kwa Kampuni iliyokamilisha vigezo vya kisheria kwa hilo sina jibu la moja kwa moja mpaka nifuatilie kumbukumbu zake"alisema Mchwampaka.
Naye Aloisi Tesha, Kamishina wa madini ambaye hivi sasa amehama anayedaiwa kushirikiana na Mbunge huyo kumikilisha eneo hilo alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa tuhuma hizo alikiri kutambua umiliki wa eneo hilo na kudai kuwa Mbunge huyo alifuata taratibu zote za kisheria za umiliki wa eneo hilo na kuwa yeye alitoa hati baada ya kuridhika kuwa amekidhi vigezo vilivyoaishwa na sheria ya Madini.
 
Mbunge aelezea
Alipoulizwa kuhusiana na malalalmiko ya wananchi hao,Mbunge wa jimbo la Liwale Faith Mtambo alikiri kuwa ana eneo anamiliki ambalo lipo katika  kijiji cha Kibutuka na kuwa amelipata kwa kufuata taratibu za kisheria na kuwa uongozi wa kijiji hicho unatambua kuwa anamiliki eneo hilo.
“Ni kweli nina miliki eneo katika kijiji hicho lakini sijawahi kuwasiliana na serikali ya kijiji wala kukutana na wananchi juu katika kupata uhalali bali kamishna wa madini kanda ya Kusini na kuwa hivi sasa anatarajia kukutana na uongozi wa kijiji hicho”alisema Mtambo na kupongeza kuwa"Mwenyekiti wa kijiji uwa nawasiliana mara kwa mara nakuwa naratajia mwezi wa saba kukutana na serikali ya kijiji baada ya kukamilisha taratibu zote kwa Kamishna wa madini"alisema Mtambo.
 Mbunge huyo alisema kuwa si shida yeye kumiliki eneo kwenye kijiji hicho kwani naye ni mkazi wa Liwale na kuwa kuna kuna vitalu vingine vipatavyo hamsini ambavyo vinamilikiwa na watu wanaoishi nje ya Liwale na kuwa jukumu lake kama mbunge pia ni kuwatafutia hao wamikili ambapo tayari ameshapata ramani na majina yao ambayo hatayawasilisha kwa serikali ya kijiji ili wawafuatilie waliko na kupata kumbukumbu zao.
"Mimi sioni kama kuna shida yoyote  ya mimi kuwa na kitalu kwenye kijiji hicho,… kwani nami pia ni mwana Liwale mbona kuna vitalu vingine hamsini vinamilikiwa na watu tena kutoka nje ya Liwale lakini hawaulizwi kwa nini mimi"alihoji Mbunge huyo.
   Mbunge huyo alisema  haoni kama ni dhambi kwa yeye kumiliki eneo kwenye kijiji hicho na vijiji vingine ndani ya Liwale kwani naye ni mkazi wa wilaya hiyo  na kuwa kuna licha yake pia vipo  vitalu vingine vipatavyo hamsini ambavyo vinamilikiwa na watu wanaoishi nje ya Liwale na kuwa jukumu lake pia ni kuwatafutia hao wamikili ambapo tayari ameshapata ramani na majina yao ambayo hatayawsilisha kwa serikali ya kijiji ili wawafuatilie waliko na kupata kumbukumbu zao.
"Mimi sioni kama kuna shida yoyote  ya mimi kuwa na kitalu kwenye kijiji hicho,… kwani nami pia ni mwana Liwale mbona kuna vitalu vingine hamsini vinamilikiwa na watu tena kutoka nje ya Liwale lakini hawaulizwi kwa nini mimi lakini nashangaa mimi kumiliki eneo imekuwa nongwa "alihoji Mbunge huyo.
Alibainisha kuwa licha ya yeye kumiliki maeneo hayo pia kuna  watu wengine wapatao 50 ambao pia wanamiliki maeneo hayo na kuwa kama Mbunge amefanya uchunguzi na kuwabaini na kuwa atawasiliana na uongozi wa kijiji cha Kibutuka ili wawaite wamiliki hao ili waonesha leseni  zao na  pia waeleze jinsi wananchi watakavyonufaika na uwepo wao.
“Mimi nakusudia kukutana na uongozi wa kijiji cha Kibutuka na vijiji vingine kwa lengo kuwatajia watu wengine ambao wanamiliki maeneo hayo kwani ni moja kati ya majukumu yangu kama mbunge wao,”alisema Mtambo.
Alisema kuwa tatizo hapo si yeye kumiliki  eneo kwenye kijiji hicho kwani ana haki kwa kuwa ni  mkazi wa Liwale  bali kikubwa ni namna gani wananchi wa maeneo  hayo jinsi   watavyofaidika na uwepo wa madini  hayo kwenye maeneo yao.
 
Sheria ya ardhi inasemaje,
Kwa  mujibu wa Sheria ya ardhi na 5, 1999,  Serikali ya kijiji  imeanishiwa kazi mbalimbali ambazo ni pamoja na kupokea, kutafakari na kuamua au kupendekeza kwa mkutano mkuu wa kijiji maombi ya ugawaji wa ardhi na rasilimali nyingine ya kijiji.
Aidha Mkutano mkuu wa Kijiji katika sheria hiyo imeweka wazi kazi zake ambazo ni Kupitisha au kukataa mapendekezo ya ugawaji wa ardhi kijijini, Kupitisha wajumbe wa Baraza la Ardhi la Kijiji, Kupitisha au kukazia mapendekezo ya wajumbe wa Kamati ya Ardhi Kijijini, Kupitisha au kukataa Mpango wa Maendeleo ya Kijiji juu ya matumizi ya ardhi na Kupokea taarifa ya namna ardhi ya kijiji inavyosimamiwa.
Kwenye sheria hiyo pia   imeanisha hatua za kufuata ambazo mwekezaji anatakiwa kufuata ambapo sheria inamtaka Mwekezaji kuwasilisha barua kijijini akielezea kiasi cha eneo analoliomba,na madhumuni ya matumizi ya ardhi anayoiomba.
Halmashauri ya Kijiji itajadili barua ya maombi na kuandika maoni yao,sababu za kukubali au kukataa kumpa mwekezaji ardhi na kupeleka maoni yao kwenye Mkutano Mkuu wa Kijiji.taarifa zinazohusiana na uhamishaji wa umiliki, pamoja na maelezo ya ardhi, maelezo ya watu watakaoathirika(kama wale watakaopoteza ardhi, ambao sasa wanamiliki kwa kufuata sheria za kimila)
Fidia kwa kijiji na wale waathirika wa moja kwa moja na mafao yoyote yatakayopatikana kijijini kwa sababu ya uwekezaji yanapaswa kubandikwa wazi sehemu zote, karibu na eneo linaloombwa.
 
Sheria ya Madini namba 14/2010 inasemaje.
Sheria ya madini imeeleza wazi  kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo na Maeneo maalum kwa leseni za awali ambapo kwenye Kifungu cha 16 kinaainisha kuwa waziri baada ya kushauriwa na bodi akiona kwa maslahi ya sekta nzima ya uchimbaji nchini Tanzania ataweza kutoa amri na kuchapisha kwenye gazeti la serikali,Kutenga eneo lolote lililo wazi na kulitangaza eneo lolote lililotengwa kwa wachimbaji wadogo kwamba limetengwa maalum kwa ajili ya watu wenye leseni za uchimbaji za awali chini ya daraja D sehemu ya nne.
 
Sheria hiyo pia inaweka Makatazo ya haki ya kuingia kwa mmiliki wa haki ya madini ambapo kwa mujibu wa kifungu cha 95 mmiliki wa haki ya madini haruhusiwi kutumia leseni aliyopewa kwa sheria hii kuingia kwenye eneo ambalo limetengwa kwa shughuli nyingine mfano shughuli za kijamii, eneo la makaburi, eneo la jeshi au eneo lolote la hifadhi mpaka apate kibali cha maandishi toka kwa waziri husika.
Vilevile mmiliki hataruhusiwa kutumia leseni hiyo na kuingia kwenye eneo bila mashauriano na serikali za mitaa ikijumuisha halmashauri za vijiji na kibali cha mmiliki halali wa eneo hilo. Pale ambapo Waziri anaona upatikanaji wa kibali kinachotakiwa unacheleweshwa bila sababu Waziri husika anaweza kutoa kibali hicho kana kwamba kimetolewa na mmiliki halali wa eneo hilo.
Kwenye maeneo ambayo yanamilikiwa na mamlaka nyingine kama hifadhi za taifa, maeneo ya reli, barabara au maeneo yaliyotolewa kwa shughuli maalum, mmiliki ataingia kwa kibali kutoka kwa mamlaka au waziri husika.SAUTI YA KUSINI

Post a Comment

 
Top