0



 HONGERA MBUNGE FAITH MITAMBO kwa kusimikwa Ukamanda wa vijana wilaya Liwale ,Maneno ya Hasani mpako 
Mwenyekiti wa ccm mkoa wa Lindi Mohamedi Mtopa akifafanua jambo kwenye  mkutano wa uvccm  wilaya  Liwale mkoani Lindi

   Na mwaandishi wetu Liwale,……
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani  Liwale  Mkoa wa Lindi wamegawanyika  makundi mawili na kusabisha uvutano na vurugu  ndani ya chama kwa kile kinachodawai kuwa ni kambi za ubunge 2015
Hayo yamebainishwa  na baadhi ya waanachama wakati walipokutana na timu ya waandishi wa habari  waliotembelea wilayani humo
Akizungumza kwa niaba ya wezake Mohamedi Mbamba alisema  kuwa  mbunge wa jimbo hilo Fairth Mitambo na  mbunge wa viti maalumu Zainabu Kawawa ndiyo chanjo cha migogoro hiyo inayosababisha kutoelewana  na kujenga  makundi ndani ya  chama hicho.
 Mbamba alisema  hali ya chama cha mapinduzi wilaya ya Liwale ni tete kutokana na kuwepo kwa  makundi yanayosababishwa na tamaa na kujali  maslai binafsi kwa  baadhi ya wanachama na watendaji wa chama hicho ngazi ya wilaya.
Aisha Nakajumwe alisema mjumbe ambaye ni mjumbe wa mkutano mkuu UWT wilaya alisema vita kati ya kundi la mbunge Faith  Mitambo  na Zainabu Kawawa ni kukombea jimbo  kwani inadaiwa kuwa Zainabu Kawawa anania ya kuomba ubunge Jimbo la Liwale
Aisha alisema kuwa hali  ya mvutano huyo unasababisha wanachama  kugawanyika sambamba na mbunge Faith Mitambo  kutozipa ushirikiano wa kutosha jumuia za chama ikiwemo ya Wazazi,wanawake na vijana  kwa madai zinatumiwa  na watu wanaotaka kugombea ubunge jimboni humo  ili kumwangusha.  
“Tabia ya mbunge wetu  sio mzuri sisi jumuia ya wazazi tumeaanda mkutano  wa baraza la  wilaya la wazazi  tulivyokwenda kwake kuomba mchango akatuambia twende kwa mbunge wetu Zainabu Kawawa we kaka majibu hayo ya  mbunge kweli ni  busara” alihoji Aisha.
Alipoulizwa  kuhusiana na madai hayo,Zainabu kawawa alisema kuwa  hakuna ubaya way eye kuomba ubunge jimbo la Liwale  ni haki yake ya msingi, kuchagua au kuchaguliwa ila muda wa kutangaza nia bado haujafika.
Kawawa aliongeza kuwa yeye ni mbunge wa viti maalumu mkoa wa Lindi  kwa hiyo ana haki ya kuwahudumia  wananchi wa  jimbo yote waliyoko  ndani ya mkoa huo,
Kwa upande wake mbunge wa jimbo hilo,Faith mitambo alisema hawezi kuongelea mambo ya chama nje ya vikao halali vya chama.
Hali hiyo inaashiria kwamba  juhudi za kumaliza mgogoro huyo zilizofanya  na kamati ya siasa ya Mkoa imegonga mwamba ambapo kamati ya siasa ilikutana  mwezi octoba  wilayani humo kumaliza mpasuko wa chama ndani ya wulaya hiy

 kamanda wa vijana Liwale mjini faith mitambo akipongezwa na katibu mwenezi ccm mkoa wa LIndi Ibrahim Mpwapwa

  
 Na  mwaandishi wetu Liwale
Makamu mwenyekiti wa Taifa wa umoja wa vijana wa CCM,Mboni Mhita amewahasa Makamanda  wa umoja wa vijana wa CCM  nchini kuzisukuma halmashauri kutoa fedha zilizotengwa na serikali kwa ajili ya vijana na wanawake.
Hayo aliyaeleza wakati wa sherehe za  kumsimika kamanda wa wilaya ya Liwale,Faith Mitambo iliyofanyika siku ya jumamosi ,ambapo alisema kuwa bila msukumo wa makamanda hao bado vijana watakuwa wanaangaika kupata mitaji wakati serikali inatenga fedha.
“Inahitajika msukumo wa mara kwa mara  kwani kumekuwa na tabia ya baadhi ya halmashauri kutumia fedha hizo kwa shughuli zingine badala ya lengo lililokusudiwa na serikali”alisema Mhita.
Alibanisha kuwa wao kama walezi wa vijana wanalojukumu la kuwainua na kuwaendeleza vijana kiuchumi na biashara ikiwa ni pamoja kuwasaidia wale wenye vipaji  mbali hasa wanamuzi chipukizi ili wanufaike na vipaji vyao.
Aidha amewataka vijana wote hapa nchi kuacha kushinda vijiweni badala yake wajishughulishe  katika shghuli za kiuchumi kwani suala la siasa ni lazima liendane na uchumi.
Akizungumza kwenye sherehe hizo ambazo pia zilizohudhuriwa na Naibu katibu mkuu wa umoja wa vijana Taifa, Hasan Mpokwa, Kamanda wa vijana wa CCM wilaya ya Liwale ambaye pia ni mbunge wa Liwale,Faith Mitambo aliahidi  kufuatilia fedha hizo  ili ziwanufaishe vijana kama ilivyokusudiwa.

MAKAMANDA wa vijana kata ya Liwale mjini na Nangando wilayani Liwale mkoani Lindi  wa kwanza Mkoyage Liwale Mjini WAPILI Kutoka Kushoto Hasani Myao diwani kata ya  Nangando

Post a Comment

 
Top