Kinachowafanya wakulima hawa kuhamia katika wilaya za Liwale na Kilwa, si kingine bali ni bei ya ufuta ikilinganishwa na ile ya zaomama la korosho ambalo wamekuwa nalo kwa miaka mingi.
Kwa kuwa korosho ni zao la kudumu, haliruhusu
kilimo cha aina nyingine hivyo wakulima hawa wa Tandahimba wanaona ni
vyema kwenda Lindi ambako kuna ardhi kwa ajili ya kilimo cha ufuta
ambacho kwa maelezo yao, wanadai kuwa “kinalipa zaidi”.
Wilaya ya Tandahimba ina wakazi 227,514 kwa mujibu
wa sensa ya watu na makazi ya 2012. Eneo hilo lina kilomita za mraba
2048.56 ambazo kati yake asilimia 90 zinafaa kwa kilimo.
Hata hivyo, asilimia 91 ya eneo linalofaa kwa
kilimo limefunikwa na miti ya mikorosho ambayo ndiyo uti wa mgongo wa
uchumi wa wakazi wake. Wilaya hiyo inayoongaza kwa uzalishaji wa
korosho, ikiwa imezalisha tani 32,000 msimu wa mwaka 2013/14.
Mkulima wa Kijiji cha Mkwiti, Mohamed Kawanga
anasema: “Ardhi yetu imefunikwa na mikorosho, ambayo ni zao la miaka
mingi, haina tena rutuba ya kuzalisha ufuta ambao unahitaji ardhi ambayo
haijachoka sana au utumie mbolea nyingi.
“Tunaenda Lindi kwa sababu kule unakuta eneo kubwa lenye ardhi nzuri, ni rahisi kuendesha kilimo hicho… Hapa kwetu ukilima, huwezi kupata chochote.”
Kawanga anasema yeye ni mmoja wa wakulima ambao
msimu wa 2013/14 walikwenda wilayani Kilwa kulima ufuta na alirejea
baada ya kuuvuna.
Anasema alilima ekari tatu na alivuna ufuta magunia manne.
“Bei yake kwa kila kilo niliuza Sh2500.
Ziliniwezesha kupiga hatua moja mbele ya maisha kwa kuwa nilipata Sh1
milioni ambayo tangu nimeanza kulima korosho sikuwahi kushika hela
nyingi kiasi hicho,” anaeleza mkulima huyo.
Naye Rashidi Liteleko (50) mkazi wa Mkwiti Juu
anasema wakulima wengi wamehamasika kulima ufuta kutokana na uwapo wa
bei nzuri na uhakika wa soko, hata hivyo nasema kukosekana kwa ardhi
yenye rutuba katika eneo lake ni kikwazo kwake.
“Napenda kulima ufuta lakini hapa kwetu wanasema
ardhi imechoka na sehemu kubwa imefunikwa na mikorosho na ndiyo maana
wenzangu wanakwenda kulima mbali, mimi sina uwezo wa kwenda kulima huko
mbali,” anasema Liteleko.
Bei ya korosho
Kawanga anasema kuyumba kwa bei ya zao la korosho kunawalazimisha kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 300 hadi wilayani Kilwa, Lindi kulima ufuta zao ambalo anasema lina bei nzuri na uhakika wa soko.
“Kila mmoja anahamasika kutokana na mafanikio aliyoyapata mwenzake. Kwa sasa hili ni tatizo kwa sababu linasababisha athari nyingine za kijamii na kiuchumi,” anasema Kilali.
“Ni kweli ufuta unahitaji ardhi yenye rutuba, hata hivyo wakulima wanaweza kuelimishwa kuhusu matumizi ya mbolea ili kurutubisha ardhi iliyochoka na wakapata mavuno mengi bila ya kuhama makazi kwa muda.”
Bei ya korosho
Katika msimu huo, wakulima waliuza korosho kwa bei
ya Sh1,000 kwa kilo moja, kiasi ambacho wanakilalamikia kuwa ni kidogo
ukilinganisha na gharama za uzalishaji wanazokadria kuwa zinafikia
Sh1,100.
Hata hivyo, takwimu za Bodi ya Korosho Tanzania
(CBT) zinaeleza kuwa gahrama za uzalishaji wa kilo moja ya korosho
inakifia Sh650.
Kawanga anasema kuyumba kwa bei ya zao la korosho kunawalazimisha kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 300 hadi wilayani Kilwa, Lindi kulima ufuta zao ambalo anasema lina bei nzuri na uhakika wa soko.
“Kama korosho zingekuwa na bei nzuri,
tusingekwenda mbali kulima ufuta. Haya yote ni baada ya kuyumba kwa zao
la korosho. Sasa tunalazimika kuangalia zao mbadala litakalotuinua
kiuchumi baada ya kushindwa kwa korosho,” anasema Kawanga.
Kaimu ofisa kilimo wa Wilaya ya Tandahimba,
Willfred Kilali anathibitisha kuwapo kwa idadi kubwa ya watu wanaoyahama
makazi yao kwa muda kwa ajili ya kwenda mkoani Lindi na kwamba idadi
hiyo imekuwa ikiongezeka kila mwaka.
“Kila mmoja anahamasika kutokana na mafanikio aliyoyapata mwenzake. Kwa sasa hili ni tatizo kwa sababu linasababisha athari nyingine za kijamii na kiuchumi,” anasema Kilali.
Hata hivyo, anasema anaamini hakuna sababu ya
wakulima wake kwenda kulima ufuta nje ya wilaya hiyo na anasisitiza kuwa
bado kuna uwezekano wa zao hilo kulimwa wilayani Tandahimba iwapo
wakulima wataelimishwa juu ya kilimo bora cha zao hilo.
“Iwapo Ufuta ungelimwa hapa, wangeuza hapa hapa na
hivyo halmashauri ingepata fedha kutokana na ushuru. Ni suala ambalo
sisi wataalamu tumeliona na tunajipanga kuwapa elimu ya kilimo bora cha
zao hilo,” anasema Kilali.
“Ni kweli ufuta unahitaji ardhi yenye rutuba, hata hivyo wakulima wanaweza kuelimishwa kuhusu matumizi ya mbolea ili kurutubisha ardhi iliyochoka na wakapata mavuno mengi bila ya kuhama makazi kwa muda.”
Naye ofisa kilimo wa Wilaya ya Kilwa, John Mkinga
anathibitisha wilaya yake kupokea wakulima kutoka Wilaya za Tandahimba,
Newala na maeneo mengine ya Mkoa wa Mtwara wanaolima ufuta.
“Wilaya imepokea wakulima kutoka wilaya za
Tandahimba na Newala wanaokuja kulima ufuta... Siwezi kutoa takwimu ni
wangapi kwa sababu tulikuwa hatujaweka mfumo rasmi wa kuwatambua. Sasa
tumeagiza viongozi wa vijiji kuwatambua wageni wote,” anasema Mkinga.“Msimu wa kilimo 2013/14 Wilaya yangu ilikadiria kulima hekta 29,652 za
ufuta, kwa sasa tumevuka lengo hilo baada ya hekta 30,100 kulimwa.
Makisio yetu ya mavuno ni tani 20,756.4 kwa wastani wa kilo 700 kwa
hekta.’’MWANANCHI
Post a Comment