Mwaandishi wetu Liwale….
Wakulima
wa kijiji cha kimambi wilaya ya Liwale mkoani Lindi wameiomba serikali
kuingilia kati mgogoro uliozuka kati ya wakulima na wafugaji baada
yafugaji kuendesha shughuli za malisho kwenye maeneo ya wakulima na
kusababisha uharibifu wa mazao.
Akizungumza
kwa niaba ya wakulima wa kijiji hicho Dalali Makanjila alisema wakulima
zaidi ya 120 wa vitogoji vya Tandawala wamevamiwa na wafugaji ambao
wametengewa eneo maaalumu la kuendeshea shughuli zao zan ufugaji,
Makanjila
alisema mgogoro usipotafutiwa ufumbuzi mapema unaweza kuleta madhara
makubwa ,hivyo ni mkuu wa wilaya tu ambaye anaweza kutatua tatizo
kutokana na watendaji na viongozi wa kijiji kuwaunga mkono wafugaji
hao,
‘’Mkuu
wa wilaya anatakiwa kufika kabla ya mambo hayajawa makubwa endapo
ataendelea kuchelewa hasira za wakulima zinaweza kuwa kali dhidi ya
mifungo na kusababisha vurugu’’alisema Makanjila
Sharifa
Kigogo alisema pamoja na kupeleka malalamiko yao kwa viongozi wa kijiji
bado kunaonekana kuna jambo la kuwalinda wafugaji hao hali ambayo
inawatia hofu wakulima kuwa kuna mchezo mchafuunachezwa na viongozi wa
serikali ya kijiji.
Kigogo
alisema wananchi wanaitaka serikali ifanye haraka kuhitisha mkutano
baina ya wakulima na wafugaji ili kuwarejesha wafugaji eneo
walilopangiwa la kuendesha shughuli zao za mifugo.
Kwa
upande wa mkuu wa wilaya Liwale Amphrey Mmbaga alisema tatizo la
wafugaji kuingia kwenye mashamba ya wakulima analitambua na ofisi yake
imeanza kulifanyia kazi ,baada ya kubaini kuwa chanzo cha mgogoro huyo
ni viongozi wa serikali ya kijiji hicho.chanzo sauti ya kusini
Post a Comment