0


    MWAANDISHIWETU LIWALE

Wanafunzi wa shule za msingi za Namihu na Nangando  wilayani Liwale mkoani Lindi wanalazimika kujisaidia vichakani kutokana na shule hizo kukosa vyoo kwa muda mrefu sasa.
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wanafunzi wa shule hizo walisema kuwa tatizo hilo limekuwa kero kwa waanfunzi kwani wakati mwingine ulazimika kukatisha masomo kutafuta  mahali pa kujisaidia ikiweo mikoroshoni.
Musa mohamedi mwanafunzi wa shule ya msingi Namihu alisema shule yao ina wanafunzi zaidi ya 200 na walimu 8 lakini hawana vyoo hali ambayo imekuwa kero kwa wanafunzi  na walimu wa shule hiyo.
Mohamedi alisema  mbali na tatizo la  vyoo pia shule inakabiliwa na upungufu wa madarasa hali inayosababisha wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tatu kusoma kwa awamu ya asubuhi na mchana.
 
Nae Fatuma Badi  mwanafunzi wa shule ya Nangando alisema kuwa shule yao inawanafunzi zaidi 300 lakini hawana vyoo vya uhakika hali ambayo inaweza kuwasabishia kupatwa na  maradhi na magongwa ya kuambukizi ikiwemo kuhara na kuhara damu.
 
Kwa upande wake diwani wa kata ya Mbaya Ali Kiyoi alisema kuwa halmashauri imetenga fedha kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa vyoo  matundu manane kwa ajili ya wanafunzi na mawili kwa ajili ya walimu.
Kiyoi aliongeza kuwa  hatua mbalimbali zinachukuliwa  ili wanafunzi waweze kusoma  katika mazingira mazuri ikiwemo  pamoja  na kuwashawishi  wazazi kushiriki kuchangia maendeleo ya elimu ikiwemo ujenzi wa miundombinu wa shule.CHANZO:SAUTI YA KUSINI

Post a Comment

 
Top