Mataifa
wahisani wamechelewesha msaada wa kuipiga jeki bajeti ya Tanzania hadi
pale uchunguzi kuhusu madai ya ufisadi katika sekta ya nishati
utakapotolewa na hatua muafaka kuchukuliwa. Kundi la wahisani hao
linalojumuisha Finland, Ujerumani, Uingereza, Norway, Sweden, Denmark,
Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, Ireland, Canada, Japan, Benki ya Dunia na
Benki ya Maendeleo ya Afrika, hadi sasa wametoa kiasi cha dola milioni
69 kama sehemu ya ahadi ya msaada wa dola milioni 558 kukidhi mahitaji
katika bajeti ya Tanzania.DW
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment