0
Kiasi ya watu 12 wameuawa baada ya treni la abiria kuligonga basi lililokuwa likivuka reli jijini Nairobi, Kenya. Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya limesema watu wengine kadhaa wamejeruhiwa kufuatia ajali hiyo mbaya iliyotokea mapema leo. Ajali za barabarani zinazosababisha
idadi kubwa ya vifo hutokea kila mara nchini Kenya. Kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria za barabara na mabasi yanayojaa abiria kupinduka, kila mara huendeshwa kwa mwendo wa kasi na kuyapita magari mengine ili kupata faida ya haraka. 

Post a Comment

 
Top