0

Wajasirimali nchini  wameiomba serikali kupunguza  urasmu  wa  upatikanaji wa  alama  ya  ubora wa bidhaa  wanazozitengeneza   ili waweze kuingia  kwenye ushindani  wa soko  la  ndani  na  nje.

Ombi  hilo limetolewa na wajasiriamali  wa walioshiriki  maonesho ya  sido  kanda  ya kusini , mashariki yanayofanyika  uwanja  wa  Ilulu  mkoani  Lindi

Isa Mkomozi Alisema kuwa  wajasirimali  wamekuwa  na  kero ya  muda  mrefu ambayo  haina  utekelezaji kwani  wajasirimali  wengi  wanashindwa  kupata  alama  ya ubora  wa  bidhaa kutoka TBS pamoja  na  huduma  hiyo  utolewa  bure

Mkomozi Alisema kitendo  cha  TBS kutokuwa   na ofisi  wilayani kuna sababisha wajasiriamali  kupata  usumbufu na  kukata tama hali  ambayo  inapelekea  bidhaa nyingi  za  wafanyabiashara  wadogo  kukosa alama ya  TBS.

 Wajasirimali  tunachangamoto  nyingi  mfano  TBS  hawapo  kila  mkoa hii  ina sababishia  kupata  usumbufu  na  kukata  tama kwani  gharama  bado  ni  kubwa ndiyo  maana  maonesho  haya  bidhaa   nyingi  hazina  alama  ya  ubora na  hata mwakani pia  utaona  hivyo hivyo Alisema

Mkurugenzi  wa  sido  Prof Eng  Sylvester  Mpanduji amewataka wananchi mkoani Lindi kutumia fursa waliyoipata ya maonyesho ya wajasiriamali wadogo na wa kati Kanda ya  kusini, mashariki  kwa kujitangaza kibiashara na kujifunza kutoka kwa wenzao ndani na nje ya nchi.

Mpanduji  aliongeza  kuwa hadi  hivi  sasa   sido  imetoa   mikopo  kwa  vikundi  vya wajasirimali  4034 nchini   wenye  thamani  ya  shilingi   billion 1.5  ambayo marejesho yake  yamekuwa  mazuri

Post a Comment

 
Top