VIJANA WALIOHITIMU MAFUNZO YA MRADI WA UWEZESHAJI VIJAN KIUCHUMI (YEE)
VIONGOZI KWENYE MAHAFALI YA MRADI WA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI
VIONGOZI KWENYE MAHAFALI YA MRADI WA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI
Na Mwandishi wetu
Vijana 264 kutoka kata za Mwenge, Jamuhuri ,Msinjahili ,Raha leo, Rasbura na Mbanja katika Manispaa ya LINDI wametunukiwa vyeti vyao baada ya kuhitimu mafunzo ya fani mbalimbali kupitia mradi wa uwezeshaji vijana kiuchumi.
Mkuu wa chuo Veta Lindi Samuel Ng’andu alisema mradi unafadhiliwa na jumuiya ya ulaya na kutekelezwa na Mashirika ya plan International Tanzania kwa kushirikiana na mamlaka ya mafunzo ya ufundi stadi VETA na shirika na VSO ,CODERT, UHIKI na Jamii.
Alisema lengo la mradi ni kuongeza wigo wa mafunzo ya ufundi stadi ili kuwafikia walengwa wengi kwa kuunga juhudi za serikali za kuwapatia ajira vijana 9100 wa mikoa Pwani,Morogoro,Lindi,Mtwara.
Ng’andu Alisema Manispa ya Lindi vijana 500 watanufaika kutoka kata 9 za mikumbi,Mitandi Mwenge Msinjahili, Jamuhuri, Mbanja, Mlandege , Makonde, Mladege na Rasbura wakati Halmashauri ya wilaya Lindi vijana 1000 watanufaika na mpango kutoka kutoka kata 9 za Nyangao , Majengo, Nyengedi, Mtua , Mtama, Kiwalala, Kitomanga, Mchinga, Kilangala, na Milola.
Alisema mradi unawalenga vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35 ambapo asilimia 53 ni wasichana na asilimia 47 ni wavulana niongoni mwao vijana wenye ulemavu asilimia 10 na wahitimu watakao patiwa vyeti ni vijana 264 wakiume 136 na wakike 128, na walemavu watatu, wakiume 2 na moja wa kike.
Post a Comment