Image captionRaia wakisajiliwa kama wapiga kura nchini Kenya mapema mwaka huu
Mahakama kuu nchini Kenya imefutilia mbali zabuni ya jumla ya $24m (£18m) ya uchapishaji wa karatasi za kura ya urais nchini humo.
Mahakama imechukua hatua hiyo ikitoa uamuzi kuhusu kesi iliyowasilishwa na upinzani kupinga utoaji wa zabuni hiyo.
Upinzani ulikuwa umesema kampuni iliyopewa kandarasi hiyo ina uhusiano na Rais Uhuru Kenyatta amabye pia anawania katika uchaguzi huo utakaofanyika tarehe 8 Agosti.
Jopo la majaji watatu limesema Tume Huru ya Uchaguzi (IEBC) ilikosa kushauriana na wagombea wote wa uchaguzi huo kabla ya kukabidhi zabuni hiyo kwa Al Ghurair ya Dubai.
Mahakama imeamua kuwa zabuni hiyo itangazwe upya.
Muungano mkuu upinzani National Super Alliance (Nasa), ulikuwa umewasilisha kesi kortini ukisema kampuni hiyo ilipewa zabuni hiyo bila utaratibu ufaao kufuatwa.
Tume ya uchaguzi ilikuwa imesema ilifuata utaratibu ufaao.
Kampuni ya Al Ghurair na Bw Kenyatta wote walikana kuwa na uhusiano wowote.
Mahakama iliamua kwamba kampuni hiyo inaweza kuchapisha karatasi za uchaguzi wa wabunge na maseneta, madiwani na magavana, ambao pia utafanyika tarehe 8 Agosti.
Mgombea urais wa Nasa Raila Odinga anashindana vikali na Rais Kenyatta, katika kinyang'anyiro ambacho ni kama marudio ya uchaguzi wa mwaka 2013.
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Ki...Read more »
kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa...Read more »
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHuenda ndege zikatengezwa bila madirisha katika siku za usoni.
Kampuni ya ndege ya Emirates imezindua nd...Read more »
Image captionMaandamano yamefanyika mjini Nairobi siku ya Jumatatu kulalamika kuhusu tuhuma za ubakaji katika shule ya Moi Girls Nairobi
Walimu pamoj...Read more »
Operesheni ya mwisho ya Tundu Lissu imefanyika na kumalizika salama.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alifanyiwa op...Read more »
Haki miliki ya pichaAFPImage captionBado muswada unahitaji kupitishwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame kabla ya kuanza kufanya kazi.
Bunge nchini Rwanda...Read more »
Post a Comment
aprieztmkrdezign
218168578325095
Emoticon
Click to see the code! To insert emoticon you must added at least one space before the code.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.