Vikundi mbalimbali vilivyoudhulia mafunzo ya kuwajengea uwezo,mafunzo yaliofanyika katika ukumbi wa halmshauri ya wilaya ya Liwale (picha na Liwale Blog)
Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Liwale mkoani Lindi ,Mary Ding’ohi akifungua mafunzo ya kuvijengea uwezo vikundi vya vijana na wanawake
Mfuko wa maendeleo ya vijana na wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Liwale mkoani Lindi umeweza kutoa mikopo ya shilingi 39,000,000 kwa vikundi 21 vyenye sifa kwa vijana na wanawake na vimetakiwa kutumia mkopo huo kwa shughuli za kiuchumi.
Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Liwale mkoani Lindi ,Mary Ding’ohi akifungua mafunzo ya kuvijengea uwezo vikundi vya vijana na wanawake
Mfuko wa maendeleo ya vijana na wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Liwale mkoani Lindi umeweza kutoa mikopo ya shilingi 39,000,000 kwa vikundi 21 vyenye sifa kwa vijana na wanawake na vimetakiwa kutumia mkopo huo kwa shughuli za kiuchumi.
Hayo yamesemwa na mgeni rasmi afisa maendeleo ya jamii wilayani
Liwale,Mary Ding’ohi wakati akifungua mafunzo ya kuvijengea uwezo vikundi vya
vijana na wanawake,mafunzo yaliyofanyika januari 19 mwaka huu katika ukumbi wa
halmashauri ya wilaya ya Liwale.
Ding’ohi amesema mikopo hiyo hutolewa kwenye vikundi vyenye sifa ambavyo vimeanza kuwa na shughuli
ya kufanya ndipo hupewa mikopo ya kuendeleza kutoka kwenye mfuko wa maendeleo
ya jamii na ametoa wito wa kuvitaka
vikundi hivyo kufanya kazi kwa bidii.
Kwa upande wake afisa jinsia wilayani hapa,Florentina Mkude
amesema vikundi vinatakiwa kuwa na tabia ya kujiwekea akiba kwenye akaunti zao
za vikundi ili kuweza kusaidia kutatua matatizo mbalimbali na kuweza kusaidia katika
kujeresha mikopo ili kuweza kuleta tija.
Nae afisa vijana Lucy Kapinga amesema miongoni wa changamoto za
vikundi vya vijana kwamba vijana wengi
wenye sifa wa kukopesheka hawajajiunga kwenye vikundi vya vijana wilayani hapa aliongeza
kusema licha ya kukabiliana na changamoto hizo amejipanga kuendelea
kuwashawishi vijana kujiunga kwenye vikundi ili kuweze kukopesheka na kunufaika.
Katika mafunzo hayo mgeni rasmi alivitunuku vyeti vikundi
4 vilivyofanya vizuri marejesho ya mkopo katika vyeti hivyo vilitunikiwa
kikundi cha City Boys kutoka kata ya Nangando,Tuinuane kutoka kata ya
Mbaya,Amani kutoka kata ya Liwale B na Nufaika kutoka kijiji cha Magereza kata
ya Mangirikiti.
Katibu wa kikundi cha Nufaika kutoka kijiji cha Magereza, Sauda
afred amesema katika shughuli zao za
ufugaji wa kuku walikumbana na changamoto za magonjwa mbalimbali lakini
changamoto hizo zimeweza kupatiwa ufumbuzi kutoka kwa maafisa ugaji kwa
kushirikiana na maafisa maendeleo ya jamii.
Sauda alisema mkopo wa awali waliweza kurejesha kwa wakati hivyo mkopo huu utawasaidia kupiga hatua zaidi kwani sasa wanauzoefu wa kutosha kusimamia mradi.
Nae Mwenyekiti wa Mtandao wa Vijana Liwale (Mvili) amesema katika mtandao huo unafanya kazi ya ufagaji wa kuku unakabiliana na changamoto nyingi ikiwemo vijana hawana mwamko wa kuchangia lakini licha ya changamoto watatumia muda wa kuwashawishi vijana kujiunga kwenye vikundi mbalimbali ili kujijengea uwezo katika kukabiliana na ukosefu wa ajila.
Mvili kwa mara ya kwanza kupata mkopo Tewelewe alisema ikiwa wao vijana watatumia elimu zao kwa kushirikiana na vijana wengi watatumia fursa hiyo ya mkopo katika kuendeleza na kuibua miradi mbalimbali na kuongeza kutoa ajili ndogo ndogo kwa vijana ifikapo juni mwaka 2017.
Vikundi 4 vilivyotunikiwa vyeti vya wakopaji bora
Picha ya pamoja afisa maendeleo ya jamii aliyekaa kwenye kiti (kulia) na vikundi vya vijana na wanawake (picha na Liwale Blog)
Sauda alisema mkopo wa awali waliweza kurejesha kwa wakati hivyo mkopo huu utawasaidia kupiga hatua zaidi kwani sasa wanauzoefu wa kutosha kusimamia mradi.
Nae Mwenyekiti wa Mtandao wa Vijana Liwale (Mvili) amesema katika mtandao huo unafanya kazi ya ufagaji wa kuku unakabiliana na changamoto nyingi ikiwemo vijana hawana mwamko wa kuchangia lakini licha ya changamoto watatumia muda wa kuwashawishi vijana kujiunga kwenye vikundi mbalimbali ili kujijengea uwezo katika kukabiliana na ukosefu wa ajila.
Mvili kwa mara ya kwanza kupata mkopo Tewelewe alisema ikiwa wao vijana watatumia elimu zao kwa kushirikiana na vijana wengi watatumia fursa hiyo ya mkopo katika kuendeleza na kuibua miradi mbalimbali na kuongeza kutoa ajili ndogo ndogo kwa vijana ifikapo juni mwaka 2017.
Vikundi 4 vilivyotunikiwa vyeti vya wakopaji bora
Picha ya pamoja afisa maendeleo ya jamii aliyekaa kwenye kiti (kulia) na vikundi vya vijana na wanawake (picha na Liwale Blog)
Post a Comment