0

 wadau  wa elimu wilayani   Kilwa  mkoani  Lindi 
 
Mwaandishi wetu
Wadau  wa  Elimu  wilaya  Kilwa  wameelezwa  kuwa Kushuka kwa kiwango cha elimu wilayani kilwa humo kunachangiwa na wazazi kutotambua umuhimu wa elimu na kusababisha kushidwa kushiriki mikakati ya kutatua cahnagmoto  za elimu wilayani humo
Hayo yamebainishwa na wadau wa elimu wilayani kilwa wakati wa kikao cha kujadili changamoto za uhamasishaji wa elimu bora kwa kutumia rasilimali za ndani
Wakitoa ushauri wao wajumbe wa kikao hicho wakiwemo wenyeviti wa kamati za shule watendaji kata madiwani na maafisa elimu kata wamesema changamoto kubwa inayosabaisha kushuka kwa elimu wilayani humo ni wazazi kutoshiriki kikamilifu katika maswala ya elimu
Mradi wa uhamasishaji wa utoaji elimu bora kwa kutumia rasilimali za ndani unaotekelezwa na action aid kwa kushirikiana na mtandao wa elimu tanzania unatekelezwa katika wilaya mbili za kilwa na singida vijijini.

Post a Comment

 
Top