0

Kuna usemi wa Kiswahili usemao, “ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo”.

Usemi huo unaweza kusawili tukio lililozuka juzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Dodoma baada ya mzazi wa mtoto anayedaiwa kupewa mimba na mwalimu wake, kuangua kilio nje ya Mahakama.

Mzazi huyo, Ayubu Mdachi aliangua kilio hicho kutokana na mwalimu Adeodatus Rutajama (30) anayedaiwa kumpa mimba mwanafunzi wake kuachiwa huru.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Mwajuma Lukindo alimuachia huru mwalimu huyo baada ya kukosekana kwa ushahidi wa moja kwa moja kumtia hatiani Rutajama kuhusika na tukio la kumpa mimba mwanafunzi wake wa miaka 15.

Post a Comment

 
Top