TIMU ya Hawili
FC (U-14) imetawazwa kuwa mabingwa wapya wa Ligi ya Jogoo leo desemba 27 baada ya timu ya Wakota fc kutofika uwanjani kucheza fainali na
kupewa pointi za mezani kwenye Uwanja wa shule ya msingi Mbaya iliyopo kijiji cha Mbaya kata
ya Mbaya wilaya Liwale mkoani Lindi.
Ligi ya Jogoo leo desemba 27 imemalizika rasmi mara baada ya kuanza kutimua vumbi Desemba 12 mwaka huu na kushirikisha jumla ya timu 4 ambazo ni mchweke fc, toto sinza fc, wakota, Hawili fc
Timu ya Hawili fc.
Hadi tunaingia mitamboni sababu halisi za timu ya Wakota
fc kutofika uwanjani bado hazijajulikana
Katika hatua ya fainali iliyokuwa ipigwe hii leo
katika uwanja wa Shule ya Msingi Mbaya Timu ya Wakota fc ilitarajiwa kuvaana
na Hawii ambao hadi muda wa mchezo
unafika haikuweza kutokea uwanjani na kupelekea Hawili fc kuibuka mshindi kwa
kuchukua pointi za mezani
Kapteni wa timu ya Hawili fc, Shanibu mandandu amesema mashindano hayo yameweza kuongeza ushirikiano mkubwa kwa wachezaji na kuibua vipaji vilivyojifisha.
Katika hatua nyengine Shanibu amewaomba wadau wa soka hapa nchini kujitokeza kudhamini mashindano mengine yanayofanana na hayo kwa lengo la kuibua vipaji vilivyojificha katika kata ya Mbaya
Katika hatua nyengine Shanibu amewaomba wadau wa soka hapa nchini kujitokeza kudhamini mashindano mengine yanayofanana na hayo kwa lengo la kuibua vipaji vilivyojificha katika kata ya Mbaya
Kwa mujibu wa mratibu wa mashindano hayo seif Kimbwanda amesema kushindwa kufika timu ya Wakota fc ni pigo kubwa kwani alitegemea fainali kuona wachezaji wakionesha uwezo wao pia ametumia nafasi hiyo kuwaomba wadau wa
soka hapa nchini kujitokeza kudhamini mashindano mbali mbali ya Vijana pindi
yanapofanyika

Post a Comment