0
Share
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 13 ya watoto huzaliwa wakiwa na uzito pungufu (Njiti) nchini Tanzania hali ambayo huchangia asilimia 86 ya vifo vya watoto wachanga.

Takwimu hizo zimetolewa jana Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Huduma za Upasuaji wa Hospital ya Taifa Muhimbili Dkt. Julieth Magandi ikiwa leo Tanzania inaungana na mataifa mengine zaidi ya 60 duniani kuadhimisha siku ya watoto njiti duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Novemba 17.

Amesema katika kuhakikisha wanapunguza vifo vya watoto njiti nchini serikali kwa kupitia Wizara ya Afya kwa mara ya kwanza wameanza kutoa dawa ya kukomaza mapafu kwa watoto waliozaliwa njiti na kuwezesha kufanikisha kupatikana kwa mashine kumi za kupumulia watoto wachanga.

Amesema kutokana na uhaba wa upatikanaji wa mashine za Oxygen, ni mashine nne pekee ndizo zinaweza kutumika kwa mara moja hali ambayo inaleta shida kwa watoto wengine kukosa huduma hiyo ikilinganishwa na idadi ya watoto wanaohitaji huduma hiyo na jitihada zaidi zinahitajika katika kuboresha mazingira ya kuwa na kitengo cha watoto wachanga mahututi Neonatal ICU.

Amesema gharama za kununulia dawa za kukomaza mapafu ni kubwa sana kwa Hospitali, idadai ya watoto ni kubwa sana ukilinganisha na nafasi za iliyopo hivyo ni watoto wachache wanaobahatika kupata huduma na uhaba wa vifaa tiba vya kutoa huduma kwa watoto hao.

Post a Comment

 
Top