0

 Mbunge wa jimbo la Kibaha vijijini Hamoud Juma wa kulia akimkabidhi madawati 537 Mwenyekiti wa halmashauri ya Kibaha vijijini Mansouri Kisebengo katika sherehe ya makabidhiano iliyofanyika katika shule ya sekondari kilanga langa.

WANAFUNZI wa shule za msingi na sekondari katika halmashauri ya Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani waliokuwa wanakabiliwa na chanagamoto ya uhaba wa madawati na viti na kusababisha baadhi yao kuwa tabia ya utoro kwa sasa wameanza kunufaika na agizo la Rais Dr.John Magufuli la kutaka wanafunzi wote nchini kuhakikisha wanasoma wakiwa wamekaa kwenye madawati.
Agizo hilo la Rais limetekelezwa na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa kupitia kupitia fedha ambazo zimepatikana kutokana na kubana matumizi yasiyo ya lazima katika ofisi yake kwa lengo la kuweza kusaidia katika kuboresha sekta ya elimu.
Akikabidhi jumla ya madawati 537 Mbunge wa Jimbo hilo kwa uongozi wa halmashauri ya kibaha vijijini katika halfa fupi zilizofanyika katika shule ya sekondari kilangalanga iliyopo Mlandizi, amesema kwamba ametoa madawati hao pamoja na vitabu kwa lengo la kuweza kupunguza kero na kuondokana na adha ambayo walikuwa wanaipata wanafunzi wa jimbo lake katika siku za nyuma.
Mbunge wa jimbo la Kibaha vijijini Hamoud Jumaa akitoa taarifa fupi kabla ya kukabidhi madawati 537 pamoja na vitabu kwa uongozi wa halmashauri hiyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais alilolitoa kwa nchi nzima la kila mwanafunzi anatakiwa asome akiwa kwenye dawati na sio kukaa chini.

Kwa upande wake Afisa elimu katika halmashauri ya kibaha vijijini Coskansia Mafuru amebainisha kwamba awali kabla ya agizo la Rais walikuwa wana upungufu wa madawati 1923 kwa shule za msingi, hivyo msaada huo utaweza kumaliza changamoto zilizokuwa zikiwakabili na kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.

Post a Comment

 
Top