Wakili mmoja nchini Marekani Joshua Neally alipelekwa hospitalini na gari lake la umeme Tesla linalojiendesha baada ya mishipa ya damu kuganda na kumsababishia uchungu mwingi kifuani.
Neally anayemiliki gari aina ya Tesla X alikuwa akielekea nyumbani kwake katika mji wa Springfield, Missouri, akitokea Branson.
Hata hivyo wakili huyo alibanwa na uchungu mwingi sana kifuani na tumboni.
Kiunyume na matarajio ya wengi alihofia kuwa angalipiga simu ya gari la huduma ya kwanza ingelimchukua muda mrefu kupata matibabu na hata labda kufa kwa hivyo akaamua kubofya kifaa cha gari lake kinachoiwezesha kujiendesha kumpeleka hospitali iliyokaribu.
'Pulmonary embolism'' ama kuziba kwa mishipa ya damu mara nyingi husababisha maafa kwani moyo unashindwa kupitisha damu na hivyo mwili unakosa hewa.
Madakta walipigwa na butwaa alipoingia katika chumba cha wagonjwa mahututi mwenyewe.
Wanasema ilikuwa ni bahati kwake kujifikisha hospitalini katika hali hiyo.
Ajali ya hivi punde zaidi ilihusisha dereva wa gari hilo na lori.
Yamkini chombo cha gari hilo kinachoiwezesha kujiendesha kilifeli kutambua kuwepo kwa lori katika barabara yake na hivyo likahusika katika ajali ya ana kwa ana.
Teknolojia hiyo ya kujiendesha sasa inafanyiwa uchunguzi wa ubora na halmashauri ya usafiri wa magari barabarani.
Joshua Neally anasema gari hilo litaokoa maisha ya watu wengi.
______________________________________
BOFYA HAPA>>>KUANGALIA RATIBA YA LIGI YA ALIZETI CUP 2016
Post a Comment