0



Zaidi ya nusu saa nilikuwa tayari nimepoteza mule ndani ni kitafakari mazungumzo yale ambayo kwa kiasi kikubwa mjomba alikuwa akilalama kuhusu tabia mbovu aliyoanzisha mkewe mwishowe kumkimbia kabisa huku akimuachia mtoto.
Mara nilianza kusikia sauti ya mama ikiniita, haraka nilijitoa mule ndani huku nikijiweka kwenye mtazamo mwingine, mtazamo ambao ingekuwa ngumu mama kujua hali yangu. Ilinibidi nijiweke vile, nilishamzoea mama yangu mara nyingi huwa ni mwepesi kubaini hali yangu, hivyo ingenisababishia maswali mengi ambayo kwa muda ule ningekosa majibu ya kumjibu. Baada ya kujihakikisha niko sawa nilijitoa ndani kana kwamba hakuna kilichokuwa kinanitatiza.
Ukweli nilifanikiwa kumhadaa mama kabla ya kuniambia nimsindikize mjomba, jambo ambalo nilikuwa nalihitaji sana maana ndio ingeweza kunipatia walau majibu ya kile kilichokuwemo kwenye kichwa changu.
Wakati huo, jua lilikuwa limebakisha masaa kadhaa kabla utawala wa giza kuingia katika usiku wa siku hiyo, hivyo miale ya jua ilikuwa imeshapoteza ubora wake, na kuleta nuru hafifu, na kuifanya kuwa jioni ya siku hiyo. Ni nyakati hizo ambazo maongezi ya mama na mjomba hayakuwa na uhai tena, baada ya kuagana hatimaye tulishika njia kutoka nyumbani kuelekea kilipo kituo cha daladala, ambazo zingemuezesha mjomba kufika nyumbani kwake kutokea mahali pale. Kituo cha daladala nacho hakikuwa karibu sana, kiasi kwamba ndio ilikuwa njia ya mimi kuweza kunipatia majibu ya maswali pindi ambapo nilipokuwa nayahitaji.
Nilimuangalia mjomba katika jicho la kuibia ibia lakini bado alionekana hayuko sawa, mtazamo wake ulionekana kubabea mambo mengi ambayo yanamsumbua katika namna moja ama nyingine, akili yangu muda huo ilikuwa ikipambana na juu ya kuuliza kile kilichokuwa ndani yangu, nilipima uzito wa lile jambo, uthubutu wa kuuliza ukanipotea huku nikikabwa kabisa, wakati huo ukimya ukitutawala miongoni mwetu baada ya maogezi machache ya hapo awali wakati tunatoka.
                                     _______
Sikuwa mtu wa kupenda kushindwa nilipokumbuka kuwa sipendi kitu kinachoitwa kushindwa jambo. Haki nilijikaza na kuufukuza ukimya katika namna ambayo mjomba hakuitegemea. Swali zito lilinitoka na kumwelekeza mjomba katika hali ya kizembe mno ya kuuliza, swali ambalo sikutegemea uwenda ningepokea majibu katika hali isiyozuilika.
Kiukweli kilio cha mjomba hakikuwa mbali, alilia sana. Kilio ambacho kiliniumiza, si kupenda hali ile niliyokuwa nikiiyona nilijitamani kujilaumu, lakini sikuwa namna njiani pale, ilininibidi nigeuke mbembelezaji, niliitahidi kuzuia kilio chake, japo kwa muda kidogo kabla ya kuendelea na safari.     
Nikiwa sitegemei kama mjomba anaweza kuniambia chochote, baada ya kunyamaza, hatimaye alianza kunijibu lile swali langu niliokuwa nimeliuliza japo ilikuwa kwa ufupi isiyoleta tija kwa upande wangu. “Ni kweli hatukuwahi kuwa na matatizo hapo nyuma na shangazi yako kama ulivyoniuliza mpwa wangu, wewe ni bado mdogo sana, ujui jinsi maisha yalivyo kimsingi kuoa uyaone”, alimaliza mjomba. Majibu ambayo yaliongeza tu maswali upande wangu na kuleta mvutano wa kile nilichokuwa nikifikiri. Sikuwa na jinsi kuhusu kukua niyaone ni kweli nilikuwa nimeshakuwa na tayari nilishaanza kuyaona. Hivyo sikutaka kuendelea na udadisi sana.
Tuliendele kupiga hatua, bahati nzuri tulikuwa tumeshasogea sana karibu na kituo cha daladala. Na hata macho yetu yaliweza kukumbana na daladala ambazo nyingi zilikuwa zimejaza watu kuliko kawaida. Tulipiga hatua chache, hatimaye pua zetu zilikumbana na harufu ya kituo kile vizuri. Ilichukua muda kidogo katika uchaguzi wa daladala ambayo ilikuwa walau ina nafasi ya kumwezesha mjomba kusimaa. Baada ya kufanikisha hilo mimi niligueza kurudi nyumbani.
                                              ********
Giza nalo lilikuwa linaingia rasmi, macho yangu yalishaanza kulipokea, ni nyakati ambazo nilikuwa, nimesharejea nyumbani. Mama akiwa anajishughulisha kuandaa chakula cha jioni, nilimchombeza kidogo katika hali ya kiutani, kama kawaida yangu.  “Mama nawe” ilinitoka huku nikiweka mdekezo wa kitoto, “mmh nini nawe ushaanza kudeka?” maneno ya mama ya kapenya kwenye masikio yangu, katika hali ya kuuliza ambayo haikuwa ikihitaji majibu kwa lazima. Tuliendelea kuzungumza kidogo. Maeneno yake ya kaleta furaja, upande wangu nilijihisi mtu katika watu. Mama alikuwa akinifurahisha sana hata hali ya unyonge kwa wakati mwingine ilikuwa ikinitoke, kutokana na vijimaneno maneno vya mama kwa wakati fulani. Nilikuwa nikijisikia raha sana Mungu kunipa mama kama yule. 
Nilingia ndani, na kuketi sebuleni, taratibu na kiendea runinga iliyokuwa ikiangaliana nami bila kuwa na uhai. Nikibonyeza kitufe cha kuipa uhai, muda kidogo ilianza kubaliana na kile nilichokuwa nataka, kukiweka nayo ikatii.    
Masikio yangu yakanza kusikia sauti ya runinga ile, huku macho ya kiona kile kilichomo ndani yake, ilikuwa ni nyimbo za wasanii wetu wa hapa nchini. Hapo kidogo zilizidi kuniliwaza na kupoteza fikra, ambazo zilikuwa zikinyanyasa kichwa changu. Muda nao haukuwa nyuma, uliendelea kwenda, nyakati hizo hurufu nzuri ambazo zilikuwa zinatoka jikoni, zilianza kunyanyasa pua yangu, huku tumbo nalo likiunguruma. Mama naye alishajua kuwa mwanae sina hali hata kidogo, muda mchache nilimwona akija, lakini katika namna nyingine.
                                                ********
Siku ya safari iliwadia hatimaye mapema tuliacha ardhi ya Tanzania, wakati huo kabla ya hapo tuliingia katika maombi mazito. Usiku wa kuamkia siku hiyo, maombi ambayo kwa upande moja ama mwingine yalizidi kunipa faraja kuhusu hali yangu. Tulimuomba Mungu atuwezeshe kufika salama ndani ya nchi ya India, na hata kuniwezesha afya yangu kuwa sawa. Hatimaye Mungu aliweza kujibu maombi yetu japo hayakuwa yote, kwa pamoja. Tuliweza kuingia India, baada ya masaa kadhaa angani ambayo sikuwa na uwakika sana yalikuwa mangapi?.
Hali ya hewa haikuwa na tofauti sana na nchini Tanzania kwa wakati ule, hivyo hakunisumbua kwa upande wangu, pia na mama. Tulikumbana na tabu pale uwanja wa ndege lakini tuliweza kufanikiwa kumpata mtu ambaye alikuwa anajua lugha ya kingereza. Hivyo iliweza kutusaidia kufanya mawasiliano, hii ilitokana na wenyeji wengi wa nchi ya India hawakuwa na kifahamu kingereza, hata Kiswahili ambazo ndizo lugha tulizokuwa tukizifahamu mimi na mama.
Baada ya kufanikiwa kumpata dereva moja wa tesi pale uwanja wa ndege ambaye alikuwa akijiua kingereza vizuri, ilikuwa msaada mkubwa sana kwetu. Aliweza kutusaidia sana kuanzia siku ile ya kwanza hadi siku ya pili tulipoelekea hospitali, ambayo haikuwa mbali na sehemu ile tulipokuwa tumefikia.
Siku hiyo ilianza ya kupendeza sana machoni mwetu, mwanga wa jua ulipenya ndani ya macho yetu na kuonesha fahari yake, hata kunifanya kuachia tabasamu ambalo ilikuwa nadra sana kwangu kuachia katika kipindi kama kile, tabasamu ambalo mwisho lilikuja kuchukizwa na siku ile iliyoanza katika, mnang’aro wa kupendeza na kuleta tumaini kwa upande wangu, hakika ilikuwa kama inanikebehi.

Post a Comment

 
Top