Kundi la wanajeshi lilikuwa limetekeleza jaribio la kupindua serikali.
Taarifa kutoka kwa kundi hilo la jeshi, ambayo ilisomwa kupitia runinga ya taifa ilisema jeshi lilikuwa limechukua mamlaka.
Mashirika ya haabri ya serikali yanaripoti kuwa majengo ya bunge mjini Ankara yamekumbwa na mlipuko wa bomu.
Kituo cha runinga cha kibinafsi cha NTV kinasema ndege ya kivita ya wanajeshi watiifu kwa serikali imeidungua helikopta iliyokuwa ikitumiwa na wanajeshi waliotekeleza jaribio la mapinduzi mjini Ankara.
- MOJA KWA MOJA: Yanayojiri kuhusu 'mapinduzi' Uturuki
- Obama na viongozi wengine wahimiza utulivu Uturuki
Lilisema nchi hiyo ingeongozwa na “baraza la amani” ambalo lingehakikisha utulivu na usalama.
Aidha, liliahidi kwamba utawala wa kikatiba ungerejeshwa “haraka iwezekanavyo”.
Alihojiwa baadaye kwenye runinga, kupitia simu na mtandao wa Facetime, ambapo alitoa wito kwa watu kujitokeza barabarani kuunga mkono demokrasia.
Marekani, Urusi, NATO na Umoja wa Ulaya wote wamehimiza kuwepo kwa utulivu na uthabiti.
Waziri wa mambo ya nje ya Marekani John Kerry amesisitiza kwamba Marekani itaunga mkono serikali ya Uturuki iliyochaguliwa kidemokrasia pamoja na taasisi zake.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.