0

                                        Kaimu mwenyekiti wa halmashauri
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Liwale , Justine Monko akiwa anatoa ufafanuzi kuhusiana na mambo mbalimbali kwenye baraza la madiwani

LIWALE, BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi limeridhia kufutwa kwa mkataba wa Kampuni ya JHS kwa kushindwa kumaliza kazi kwa muda mwafaka . 

 Maamuzi hayo yalifanyika Julai 27 katika Kikao cha mwaka cha baraza la madiwani lililofanyika ukumbi wa Halmashauri, huku madiwa wakidai kampuni hiyo imeshindwa kufanya kazi kwa wati hivyo inaweza kuisababishia halmashauri hasara kubwa. 

 Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Liwale , Justine Monko alisema ipo haja ya kufuta mkataba na kampuni ya JHS kufanya kazi na Halmashauri kwakuwa kampuni hiyo imeshindwa kufanya kazi katika muda mwafaka huku akisena dawa ya jipu ni kulitumbua.

 Pia, baraza hilo liliazimia kumsimamisha kazi mwandisi wa ujenzi wa halmashauri kwa kushindwa kusimamia baadhi ya miundombinu ya barabara zilizopokelewa huku zikiwa zimejengwa chini ya kiwango Licha ya madiwani wa kata ya Liwale mjini kukataa barabara hizi kwa kujengwa chini ya kiwango. 

Hata hivyo baraza liliamua  na kumpa onyo kali ya mwisho mwandisi huyo kwa kumwambia anatakiwa kufuatilia kwa ukaribu na kwa umakini kuanzia sasa.

 Diwani wa kata ya Nangando,Jafari Mkungu alisema kwenye kata yake kuna barabara ya mita 400 ya Kambarage iliyopo katika kijiji cha Mbonde kata ya Nangando ambayo imejengwa chini ya kiwango nae diwani wa kata ya Liwale mjini Adamu Mahekula aliikaa kuipokea barabara ya mita 850 ambayo ya kutoka kwa tengeneza hall mpaka kwa msikiti wa Mbinga iliyojengwa chini ya kiwango pia. 

Baraza lililalamikia kuwepo kwa madawati yasiyo na kiwango hiyo wameitaka halmashauri kuhakikisha mkandarasi aliopewa tenda hiyo kutolipwa kwanza pesa mpaka pale ayafanyie marekebisho madawati yote yaliotengewezwa chini ya kiwango kwa ghalama yake.

 Diwani wa viti maalu,Siwema Mbogo waliwatupia lawama wakuu wa idara kwa kushindwa kutoa taarifa zao kwa umakini hiyo amewata wakuu hao wa idara wawe makini katika utoaji wa taarifa zao hatua hii ilifikia baada ya kuwepo taarifa mbili tofauti za kuwepo idadi sahihi ya madawati katika shule ya msingi Tepetepe. 

 Katika baraza hilo katika halmashauri ya wilaya inaonesha hakuna watumishi hewa lakini mkurugenzi wa halmashauri,Justine Monko hawezi kuipeleka yake kwenye kisu hivyo alisema zoezi la uhakiki wa watumishi hewa litarudiwa tena ili kuweza kujirizisha richa ya ofisi yake kukuta taarifa ya watumishi hewa 0.

Post a Comment

 
Top