0


Rais Obama anayehudhuria mkutano huo anatarajiwa kufanya ziara ya kihistoria ya kuwa rais wa kwanza wa Marekani kuzuru eneo la Hiroshima ambalo Marekani ilifanya shambulizi la kwanza kwa bomu la atomiki nchini Japan.
Mkutano wa viongozi wa mataifa saba tajiri kiviwanda umeanza Alhamisi katika mji wa Ise Shima nchini Japan. Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amewahimiza viongozi wa mataifa hayo kutafuta suluhisho bora kukabiliana na hali ya uchumi wa dunia unozidi kufifia. Suala kuu linalotarajiwa kupewa kipaumbele kwenye mkutano huo ni hali ya uchumi duniani pamoja na ushirikiano katika vita dhidi ya ugaidi.
Kabla ya mkutano huo kuanza waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe alisema "Kauli mbiu kuu katika mkutano ni jinsi mataifa ya G7 yataitikia hali ya sasa ya uchumi duniani. Huu ndio wakati wa mataifa ya G7 kushughulikia hali mbalimbali na ninayo matumaini mkutano utapitisha ujumbe thabiti na bayana unaojumuisha kuimarisha uchumi thabiti wa ulimwengu"
Hata hivyo huenda muafaka ukakabiliwa na ugumu ikizingatiwa Kansela wa Ujerumani Angela Merkel alishakataa wazo hilo, wawili hao walipokutana mapema mwezi huu. Shinzo Abe anasema
Rais Barack Obama na waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe.
Rais Barack Obama na waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe.
Rais wa Marekani Barrack Obama anayehudhuria mkutano huo anatarajiwa kufanya ziara ya kihistoria ya kuwa rais wa kwanza wa Marekani kuzuru eneo la Hiroshima ambalo Marekani ilifanya shambulizi la kwanza la bomu la atomiki tarehe 6 Agosti mwaka 1945. Inahofiwa kuwa ziara hiyo ya Obama Hiroshima huenda ikapata umaarufu zaidi na kuumeza mkutano wenyewe.
Suala jingine linalotarajiwa kupewa kipaumbele ni vita dhidi ya ugaidi ambapo rais wa Ufaransa Francois Hollande anatarajiwa kuzungumzia mashambulizi mawili ya kigaidi dhidi ya nchi yake mwaka jana.
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron anahudhuria mkutano huo huku suala la nchi yake kupiga kura ya maamuzi mwezi ujao kujitenga au kusalia katika Umoja wa Ulaya likitarajiwa kujipenyeza kwenye mkutano huo.
Viongozi wengine wanaohudhuria mkutano huo ni kansela wa Ujerumani Angela Merkel, rais wa Ufaransa Francoise Hollande, kiongozi wa Italia Matteo Renzi na wa Canada Justin Trudeau.
Maafisa wa Japan wamesema wameimarisha usalama huku maelfu ya polisi wakishika doria katika maeneo na vituo mbalimbali.

Post a Comment

 
Top