0

Watu wa Jamii ya Wawindaji, warina asali,  na waokota matunda pori kutoka kabila la Wahadzabe wanaoishi katika bonde la Yaeda chini wilaya ya Mbulu wanakabiliwa na tatizo la njaa kali inayodaiwa kusababisha baadhi ya wanaume kuzikimbia familia zao na kuiomba erikali na taasisi binafsi zenye uwezo wa kusaidia kupatikana kwa chakula ziwasaidie kupunguza adha hiyo.Wakizungumza na Ripota wetu wazee wa jamii hiyo katika kijiji cha Mongoamono wamesema hali imekuwa mbaya kwa upande wao na watoto ambao ndiyo waathirika wakuu na inadaiwa imesababishwa na mabadiliko ya tabia nchi yanayochangiwa na uharibifu wa mazingira unaofanywa na watu kutoka jamii nyingi na kwamba hawana njia mbadala ya kupata chakula.

Kwa upande wao baadhi ya vijana  wamesema hivi sasa wanalazimika kuchimba mizizi hata isiyoliwa ili kuokoa uhai wao,watoto na wazazi wao kwani hakuna matunda wala wanyamapori kama walivyozoea

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mongoamono Kata ya Yaeda chini Bw. Pascal Kajema amesema uongozi umeanza kutoa elimu kwa jamii hiyo  ili  kubadili mfumo wa maisha yao waweze kujihusisha na shughuli  zingine zikiwemo za kilimo ili kukabiliana na tatizo njaa.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top