UPORAJI WA PIKIPIKI WATIKISA LINDI
NA Fadhila Mwanja,Lindi
Uporaji wa pikipiki umeitikisa mkoani Lindi
kutokana na matukio ya kikatili 34 yametokea ndani ya
miezi mitatau tangu januari
hadi machi mwaka
huu.
Hayo yamebainishwa
na mkuu wa upelelezi wa jeshi la polisi nchini DCI
Diwani Athuman wakati alipokuwa anazungumz a na waandishi wa habari kwenye ziara yake ya
kikazi mkoani hapa.
Athumani amesema kuwa
matukio ya uporaji wa pikipiki mkoani
humu yamekuwa tishio
kwa maisha ya waendesha pikipiki na abiria kwani
yameongezeka kutoka 11 mwaka 2015
hadi 34 marchi 2016.
Alisema serikali
haiwezi kuwavumilia waalifu hao wakiendelea kufanya matendo ya
unyanyanyi na ukatili dhidi ya
binadamu mwengine ambao wanaangaika kutafuta riziki zao kwa njia halali.
Athumani alisema pia idara yake haitawavumilia askali polisi idara
ya upelelezi wenye tabia ya uomba na
kupokea rushwa kwa lengo la kuchelewesha
na kupotosha ukweli katika kesi kwa visingizo mbalimbali.
Aidha alisema seriklai ya awamu tano imejipanga na imejidhatiti kwenye ukusanyaji wa kodi hivyo jeshi la polisi lita hakikisha bandari bubu
zote zinadhibitiwa ili kupunguza mianya
ya ukwepaji kodi unaofanya na wafanyabiashara wasio wadilifu,Ndugu zangu suala la kodi ni uti wa mgongo wa taifa lolote duniani kw nafsi
hii nawaomba wale wote wanaotumia babdari bubu
kukwepa kodi kuacha mara
moja kabla mkono wa sheria
hawajakutanao alisema Athumani
Kamishna wa makosa ya jinai kwa jeshi la Polisi wa Taifa, Diwani Athumani akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Lindi Jana.
Post a Comment