0
              
Liverpool yatinga nusu fainali baada ya ya kushinda 4-3 dhidi ya Borrussia Dortmund
Hatua ya Robo fainali ya michuano ya Europa imeendelea tena Alhamisi kwa michezo minne, ambapo Liverpool imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali kufuatia ushindi wa mabao 4 -3 dhidi ya Borrussia Dortmund.
Magoli ya Liverpool yamefungwa na wachezaji Divock Origi, Philippe Coutinho, Mamadou Sakho na Dejan Lovren.
Na magoli ya Dortmund yamefungwa na Henrikh Mkhitaryan, Pierre-Emerick Aubameyang na Marco Reus .
Sevilla imeiondoa Athletic Bilbao kwa changamoto ya penalti 5-4 kufuatia sare ya jumla ya 3-3 baada ya kila timu kushinda 2-1 mechi ya nyumbani.
Villarreal imeifunga Sparta Praga bao 4- 2 na Shakhtar Donetsk imeirarua Sporting Braga kwa mabao 4-0.
Kwa matokeo hayo Liverpool inaungana na Sevilla, Shakhtar Donetsk na Villarreal katika hatua ya nusu fainali.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top