0

Watoto zaidi 1,194 ambao wameandikishwa kuanza darasa la kwanza mwaka huu katika shule tano za msingi ndani ya kata ya Kianyari wilayani Butiama mkoani Mara wanalazimika kutumia viwanja vya michezo kama madarasa baada ya shule hizo kukabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa.
Akizungumza katika kikao cha maendeleo ya kata ya Kianyari, mratibu wa elimu kata hiyo Bw George Bigori, amesema wastani ya watoto mia moja hadi mia tatu wameandikishwa kuanza darasa la kwanza kwa kila   shule ya msingi katika kata kianyari, idadi ambayo amesema imekuwa   kubwa ukilinganisha na vyumba vya madarasa vilivyopo. 
                                   
Hata hivyo mratibu huyo wa elimu katika kata hiyo ya Kianyari, amesema kuwa pamoja na wazazi kutakiwa kuchukua hatua zinazolenga kupunguza baadhi ya changamoto katika shule hizo, lakini pia halmashauri ya wilaya ya Butiama kupitia idara ya elimu imetangaza kuchukua hatua kali kwa walimu wakuu ikiwa ni pamoja na kuwavua nyadhifa zao endapo itabaini kuna mwanafunzi amefika darasa la tatu bila kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Post a Comment

 
Top