NA Mwandae Mchungulike,Liwale
Mbunge viti maalum wa Chadema mh,Lathifa Kigwalilo Jana
februari 27,mwaka 2016 alitembelea
gereza la Kilimo Kipule lililopo katika kijiji cha Kipule Mangilikiti wilayni Liwale
Mkoa wa Lindi ambako alipata nafasi ya kuzungumza na wafungwa na kuwapatia msaada
wa vitu kama sabuni,miswaki pamoja na dawa za meno ambazo huduma hiyo walikuwa
wamekosa kwa muda mrefu sasa.
Katika ziara hiyo alizikuta Changamoto nyingi sana baadhi ikiwa ni;ukosefu wa Maji safi na Salama hakuna hali ambayo inaweza kusababisha
kusambaa kwa magonjwa ya mlipukoUmeme hakuna katika eneo la wafungwa,umeme wa
rea umeishia nje ya magereza katika nyumba za askari magereza Mesi ya chakula imeezekwa na makuti Vyoo vichache na sio vya viwango kabisa,uzio Ukuta wa miti,Wafungwa hawana ndala,Chawa na kunguni kutokana na kukosa dawa za fumigation kwa
wakati.
Mbunge akiwafaraji wagonjwa jana katika ziara yake alipotembelea katika hospitali ya wilaya ya Liwale
Pia katika ziara yake alitembelea katika hospitali ya wilaya
ya Liwale iliyopo Mkoa wa Lindi alipowatembelea wagonjwa ambako alitoa msaada wa
chandarua katika wodi ya wazazi na alipata fursa ya kuzungumza na kila mgonjwa
kwa kuwafariji.
mbunge akikagua mradi wa umwagiliaji uliopo katika kijiji cha Mtawango kata ya Mbaya wilayani Liwale
Mbunge akitoa maelezo kwenye ujenzi wa umwagiliaji ambao ujenzi wake haujakamilika
Akiwa katika kijiji chaMtango kata ya Mbaya wilaya ya Liwale
Mkoa wa Lindi ambako alikagua ujenzi wa nyumba ya wauguzi ambayo hadi ilipoanza
kujenga kwa kipindi kirefu hadi sasa bado ujenzi wake haujakamilika.
“Wananchi wanalazimika kuchangishana kulipia kodi ya
wauguzi Pia na mradi wa
umwagiliaji ambao ujenzi wake pia haujamalizika hadi leo na haujajengwa katika
kiwango”alisema Kigwalilo
Mbunge viti maalum akikabidhi msaada wa jezi na mipira kwenye uwanja wa wilaya ya Liwale ambapo jana kulikuwa na ufunguzi wa Ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa katika kituo cha LiwaleMbunge viti maalum akikabidhi msaada wa jezi na mipira kwenye uwanja wa wilaya ya Liwale ambapo jana kulikuwa na ufunguzi wa Ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa katika kituo cha Liwale
Mbunge viti maalum akikabidhi msaada wa jezi na mipira kwenye uwanja wa wilaya ya Liwale ambapo jana kulikuwa na ufunguzi wa Ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa katika kituo cha Liwale
Mbunge ameweza kuchangia kuhodhi kituo cha michezo kilichopo
katika wilaya ya Liwale kwa kukiwezesha kituo hicho kuendesha ligi ya daraja la
tatu ngazi ya mkoa jana kwenye ufunguzi
wa mashindano hayo aliwapatia kila timu jezi na mipira kwa timu tatu za Liwale
zinazoshiriki mashindano ya ligi hilo.









Post a Comment