0
Dk Shein akishuka katika gari la kijeshi alilotumia kuwasalimia wananchi
Mamia ya wananchi wa mikoa mitano ya Unguja wamejitokeza kwa wingi kusherehekea
miaka 52 ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kufurika kwa wingi katika uwanja wa Amaan
mjini hapa.
 
Maandamano ya wananchi wa mikoa mitano ya Unguja waliopita mbele ya mgeni rasmin
rais wa Zanzibar  dk.Ali Mohamed Shein na wageni mashuhuri,ngoma ya asili za
utamaduni wa watu wa Unguja na gwaride rasmin la vikosi vya ulinzi vikiongozwa na
jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ,ni baadhi ya matukio yaliyowavutia wananchi wengi
waliofika katika kiwanja cha Amaan.
 
Wananchi walianza kuingia katika uwanja wa Amaan kuanzia majira ya saa moja ambapo
milango ilianza kufunguliwa na kuruhusu wananchi ikiwemo waliotoka katika kisiwa cha
Pemba hadi kufika saa 4 ulionekana wazi wazi kuzidwa na idadi kubwa ya wananchi
ambao walibaki nje ya uwanja.
 
Meli mpya ya MV.Mapinduzi ilifunga safari kwenda katika kisiwa cha Pemba kwa ajili
ya kuchukuwa wananchi ili kupata nafasi ya kuhudhuria sherehe hizo
 
'Yadumu mapinduzi ya Januari 1964 ni maneno yaliyoandikwa katika baadhi ya mabango
yaliyobebwa na waandamanaji waliopita mbele ya mgeni rasmin wakimaanisha kwamba
watayalinda mapinduzi kwa nguvu zote.
 
Viongozi maarufu wa kitaifa walianza kuingia katika majira ya saa 2.30 ambapo
viongozi waliotia fora na kushangiliwa kwa nguvu zote ni rais wa jamhuri ya muungano
wa Tanzania John Magufuli ambaye mara tu alipoingia alipigiwa wimbo wa taifa.
 
'Hapa kazi tu'ni sehemu ya kauli zilizosikika kutoka kwa wananchi ambao
walimkaribisha rais Magufuli ambaye hiyo ilikuwa mara yake ya wanza kuhudhuria
sherehe za Mapinduzi akiwa rais wa Muungano.
 
Baadhi ya wananchi waliohojiwa walikiri na kusema sherehe za miaka 52 zimefana licha
ya wafuasi wa chama cha CUF wakiongozwa na makamo wa kwanza wa rais maalim Seif
Sharif Hamad kususia.
 
Maalim Seif Pamoja na mawaziri wanaounda serikali ya umoja wa kitaifa kutoka CUF
wamesusia sherehe hizo kwa kile kinachoelezwa kutoridhishwa na maamuzi ya tume ya
uchaguzi ya zanzibar ZEC kufuta uchaguzi wa Oktoba 25.

Baadhi ya Maafisa mbali mbali wa Vikosi vya Ulinzi na Taasisi za
Serikali wakiwa katika sherehe za kilele cha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
kutimia miaka 52 zilizofanyika leo katika uwanja wa Amaan Studium Mjini
Unguja
Vijana wa Chama cha Mapinduzi wakibeba Picha la Marehemu Rais wa
Kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Karume wakati wa Maandamano ya kusherehehekea
Kilele cha Mapinduzi Kutimia miaka 52 leo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali
Mohamed Shein akikagua gwaride la Vikosi vya Ulinzi liliandaliwa rasmi katika
kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya
Zanzibar,zilizofanyika leo katika Uwanja wa Amaan Studium Mjini
Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali
Mohamed Shein akiteta na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John
Pombe Magufuli wakati wa kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi
Matukufu ya Zanzibar,zilizofanyika leo katika Uwanja wa Amaan

Post a Comment

 
Top