0



Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Simon Sirro akionesha kwa waandishi wa habari baadhi ya silaha zilizokamatwa na Jeshi la Polisi katika oparesheni inayoendelea ya kukabiliana na wimbi la uhalifu.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam amewatahadharisha wananchi kutobeba kiasi kikubwa cha fedha kutoka benki bila kuwa na ulinzi.
Ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu operesheni kali inayoendelea ya kukabiliana na wimbi la uhalifu.
Kamishna Simon Sirro amewasisitiza wananchi kuacha tabia ya kuchukua kiasi kikubwa cha fedha kwakua wanatahadharisha maisha yao.
“kuna namna nyingi za kuhamisha fedha zikiwemo za kutumia mitandao ya simu,ni vizuri kutumia njia hizo kuliko kubeba fedha mkononi bila ulinzi”alisema Sirro.
Aidha, Kamishna Sirro amewataka wananchi wanaochukua fedha kwa kiasi kikubwa kutoka benki wasindikizwe na polisi ili kulinda usalama wao na mali zao
.
Pia ametoa rai kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za waalifu ili kuondoa wimbi la uhalifu linaloendelea kushamiri siku hadi siku.
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam linaendesha oparesheni katika mikoa yote ya kipolisi iliyoanza mwishoni mwa mwezi Desemba ambayo inahusisha ukamataji wa majambazi, waporaji wa kutumia pikipiki na wahalifu wengine.
Source: Jacquiline Mrisho MAELEZO

Post a Comment

 
Top