"Mumeniomba niongoze nchi hadi baada ya 2017. Kwa kuzingatia umuhimu wa hili kwenu, sina budi ila kukubali,” alisema Bw Kahame kwenye ujumbe wake uliopeperushwa moja kwa moja kupitia runinga.
Hata hivyo aliongeza kwamba hakusudii kuongoza Rwanda hadi kufa kwake.
Hii ni siku chache baada ya kufanyika asilimia 98 ya Wanyarwanda kuidhinisha marekebisho ya katiba ya kumruhusu Bw Kagame kuwania tena.
Kura hiyo ilifanyika mwezi uliopita.
Mabadiliko hayo, ambayo yanamuwezesha kiongozi huyo kutawala hadi mwaka 2034 imeshutumiwa na Marekani na mataifa mengine ya magharibi.
Amesifiwa kwa kurejesha uthabiti katika taifa hilo na kuendeleza ukuaji wa kiuchumi baada ya mauaji hayo.
Lakini wakosoaji wake wanasema yeye ni kiongozi wa kiimla ambaye huwa hawavumilii wapinzani. Ametuhumiwa pia kwa ukiukaji wa haki za kibinadamu, madai ambayo amekanusha.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.