Jeshi la Polisi mkoani Geita linawashikilia watu wanne wanaodaiwa kuhusika na kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani humo, Alphonce Mawazo.
Kifo cha marehemu Mawazo kimetokea jana Jumamosi Novemba 14 majira ya saa sita mchana baada ya kuvamiwa na kundi la watu na kuanza kumshambulia kwa silaha za jadi.
Alphonce Mawazo akiwa na Godbless Lema.
Ameongeza kuwa tatizo hilo kutokea kunahusishwa pia na itikadi za kisiasa lakini bado Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wake.
Hata hivyo Kamanda Mponjoli amesema hali ni nzuri maeneo ya Katoro hasa Kata ya Ludete ambapo uchaguzi wa diwani umefanyika leo.

Post a Comment