Na Mwaandishi wetu Nachingwea
Chama cha walimu(CWT) wilaya ya
Nachingwea,mkoani Lindi kimefanya uchaguzi na kuwapata viongozi
watakaokiongoza chama hicho kwa muda wa miaka mitano huku wakimchagua
tena,Bakari Ngualo kuwa mwenyekiti.
Kwa mujibu wa Katibu wa wilaya wa
chama hicho ,Aidan Mahelela alisema kuwa katika uchaguzi huo uliofanyika
hivi karibuni na kusimamiwa na mjumbe wa kamati ya utendaji Taifa,Dionis
Mbilinyi ulimchagua tena Johari Abdalah kuwa mweka hazina.
Mahelela iliwataja wengine
waliochagua kuwa ni pamoja na Kerubina Mungurumo ambaye ni mwakilishi
kitengo cha wanawake wa sekondari,Hasani Mpwapwa mwakili wa walemavu na Yonas
Rashidi mwakilishi a vijana.
Wengine ni Manufred
Mmuni mwakilishi upande wa uongozi wa idara ya elimu,Dismas Nivahe
mwakilishi wa chuo cha walimu,Fatuma Ayuba mwakilishi wa shule za
awali,Hadija Ngawina na Joseph Kakinga wawakilishi wa sekondari.
Akizungumza kwenye mkutano huo wa
uchaguzi Mjumbe wa kamati ya utendaji Taifa wa CWT,Dionis Mbilinyi alito mwito
kwa walimu kununua hisa ya benki ya walimu ambazo zimeanza kuuzwa kwenye benki
za CRDB na kampuni ya Max malipo Africa.
“ Natoa wito kwa walimu
wote mujitokeze kununua hisa ya benki yetu ya walimu kwani ndio itakuwa
mkombozi wetu hasa katika kujipatia mikopo”alisema Mbilinyi.SOMA ZAIDI
Post a Comment