0

Waziri wa Nishati na Madini,George Simbachawene akipewa maelekezo leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Felshesm Mramba kuhusiana na uboreshaji wa Mtambo wa umeme uliopo katika wizara ya Nishati na Madini.
Waziri wa Nishati na Madini,George Simbachawene akikagua Mtambo wa umeme uliopo nyuma ya jengo la Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.

Mitammbo ya umeme iliyopo nyuma ya jengo la Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
IFIKAPO machi mwakani tatizo la umeme jijini Dar es Salaam itakuwa historia kutokana na kukamilika kwa miundombinu ya mitambo ya umeme ifikapo machi mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini,George Simbachawene katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya umeme ya Kurasini, Mbagala pamoja na Kinyerezi jijini Dar es Salaam leo.
Ziara hiyo iliyoanzia katika mitambo ya Umeme Wizarani hapo na kuelekea,Kurasini na Mbagala ikiwa na lengo la kusogeza miundombinu ya umeme karibu na watumiaji wa umeme.
Simbachawene amesema kuwa kuna miradi minne ambayo mpaka sasa inafanyiwa kazi kwa uhakika inayotegemewa kusambaza Umeme kwa watumiaji bila kuwa n amatatizo ya umeme.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Felshesm Mramba amesema kuwa matatizo mbalimbali ya ununuzi wa Luku za umeme nayo yanafanyiwa kazi kwa kuyahimiza makampuni nayoshirikiana na TANESCO katika uuzaji wa umeme ili waweze kuimarisha huduma hizo.

Post a Comment

 
Top