0
         
Nembo ya Tume ya Uchaguzi Tanzania, chini yake ni mwanamke mmoja akimsaidia mwenzake kumwonyesha sehemu ya kupiga kura
Tume ya uchaguzi nchini Tanzania imesogeza mbele kwa wiki moja zaidi tarehe ya kuzinduliwa kwa zoezi la daftari la wapiga kura litakalotumia mfumo mpya wa kieletroniki yaani Biometric Voters Registration BVR. Zoezi hilo ambalo litaanza rasmi katika mkoa wa Njombe na baadae kufuatia katika mikoa mengine ya Tanzania hivi sasa linatarajiwa kuanza tarehe 23 ya mwezi huu badala ya tarehe 16 kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini humo amesema lengo la mabadiliko hayo ni kuvipa fursa vyama vya kisiasa kujiandaa na kuandaa watu wake. Hata hivyo, baadhi ya viongozi wa vyama vikuu vya kisiasa wamesema kauli hiyo haina ukweli wowote na kwamba tume inajikosha kwa sababu haina vifaa vya kutosha vya kuendesha uandikishaji huo.KUSOMA ZAIDI HABARI HII BOFYA HAPA

Post a Comment

 
Top