0

Hakimu wa mahaka ya wilaya kilwa mkoani Lindi Mr chuya akifafanua jambo kwa  wananchi walioshiriki maadhimisho ya siku ya sheria iliyofanyika wilayani humo juzi
 maadhi misho ya siku ya sheria kilwa mkoani Lindi

Mwaandishi wetu 

Wananchi wilaya ya  Kilwa mkoa wa Lindi wametakiwa kutii na 
kutekeleza matakwa ya sheria ili kuhakikisha haki ya kila mtu 
inatendeka na kuweza kuishi bila kubughudhiwa na mtu.
Hayo yameelezwa leo Kilwa masoko na hakimu mkazi
 mfawidhi wa
 mahakama ya wilaya ya Kilwa mkoani Lindi,Arcard 
Chuwa,kwenye 
sherehe ya maadhimisho ya siku ya sheria duniani.
Chuwa alisema kila mtu anawajibu wa kutii na kutekeleza matakwa 
ya sheria zilizowekwa ili kila raia aishi katika njia ambazo hazita 
wabugudhi na kuwadhulumu raia wengine.
Alisema mahakama hazina haki ya kukataa sheria zilizotungwa na
 bunge kwani chombo hicho  kinawakilisha wananchi,hivyo kama
 sheria imetungwa ni dhahiri wananchi wenyewe wameitaka na 
kuiridhia sheria hiyo.
Chuwa alisema ilihaki iwepo ni lazima  kuwepo na sheria nzuri  
na za haki,hivyo ni wajibu wa mahakama,serikali  na wadau 
wengine kuhakikisha sheria inafuata misingi ya haki." haki ni
 jambo muhimu katika kuchunguza chanzo cha sheria  na 
kusimamia  :
wake,kama haki haipo itakuwa ni sheria yenye nguvu tu
"ndiyo maana marehemu Shaaban Robert alisema waweza 
kuichovywa hatia yako katika dhahabu upendavyo lakini 
mkuki imara wa haki hauvunjiki,"alisema Chuwa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya
 Kilwa Ali Mtopaalisema walisema udhaifu katika kutoa
 hukumu
 unasababisha raia kujichukulia sheria mkoni.
 Ali Mtopa alisema hukumu zisipotolewa kwa haki zinakuwa
 ni chanzo cha wananchi kujichukulia sheria mkononi baada
 ya kuona maamuzi yaliyotolewa yanawafanya wahalifu kuwa 
huru na kuendelea kutenda uhalifu.

Post a Comment

 
Top