0
Timu ya Taifa ya Ivory Coast imetwa Kombe la Mataifa barani Afrika AFCON 2015 baadaya kuifunga Ghana kwa penati 9 kwa 8 katika mchezowa Fainali.
Katika mchezo huo timu hizo zilishindwa kufungana katika dakika zote 120 na baada ya kuingia katika hatua ya penati timu zote zilikosa penati 2 katika penati 5 za kwanza na kulazimu mikwaju kuendelea mmoja baada a mwingine ambapo hatimaye wachezaji wote 11 wakapiga penati.
Golikipa wa Ghana Brimah Razak aliyepiga penati ya 9 ndiye aliyekosa kwa mkwaju wake kupanguliwa na kipa wa Ivory Coast Boubacar Barry ambaye kwa upande wake alifunga penati ya 9 na ya ushindi.
Christian Atsu wa Ghana ndiye aliyepata tuzo ya Mchezaji bora na tuzo ya bao bora la mashindano hayo ya mwaka huu.
Fainali hii imekumbushia ile ya mwaka 1992 ambayo Ivory Coast walishinda kwa penati 11 kwa 10.

 


 Sammy Kuffour kanyolewa nywele live studio baada ya kuahidi kunyolewa kama Ivory Coast itaifunga nchi yake Ghana katika fainali


 

Post a Comment

 
Top