0

mwaandishi wetu Liwale….
 Baadhi ya Wananchi wa Liwale mkoani Lindi   wamesema  wamekataa tamaa   na hali ya maisha ya yao kutokana na kukosa huduma  muhimu zap  kijamii ikiwemo  maji safi, mawasilino na huduma bora za afya
Akizungumza kwa niaba ya  wananchi wa kijiji cha Ngunja na  Lilombe wilaya humo  Mwajuma   Mkombe  alisema kuwa  maisha ya  wananchi yamekuwa ya kubahatisha  kama wanyama  kila kukicha hali inakuwa ngumu  afadhali ya jana kwani, kilimo kama nguzo kuu ya kiuchumi kwao, kimekuwa hakiwaletei tija yoyote.
“Ni hatari ukifika vijiji  vya Ngunja, Lilombe, Ngogowele ukawauliza wakulima wanachohitaji utawasikia wakilalamika shida yao ni ukosefu wa soko la uhakika la mazao na uhaba wa pembejeo. Mawasiliano na huduma za kijamii, afya na maji.
Hawajui nani atawajibika kuwalipa japo fidia kidogo ya hasara waliyopata. Baada ya kukosa soko la uhakika mazao yao ikiwemo korosho mahindi na upunga,upande wa elimu, ni shida shule chache, walimu hawatoshi, maabara hakuna huku umbali ukiwa kikwazo kwa wanafunzi wa baadhi ya maeneo," alisema

Post a Comment

 
Top