0
Shirika la Hisani la Madaktari Wasio na Mipaka – MSF limesema litazindua majaribio ya kliniki ya aina tatu ya dawa za kutibu ugonjwa wa Ebola katika eneo la Afrika Magharibi kuanzia mwezi ujao wa Desemba. Majaribo hayo yatafanyika nchini Liberia na Guinea. Ni habari za kuwapa matumaini wagonjwa katika juhudi za kutafuta dawa kamili ya Ebola, ugonjwa hatari unaoua kati ya asilimia 50 na 80 ya watu walioambukizwa.

Post a Comment

 
Top