0

Serikali imetenga bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwaajili ya kununua vifaa vya maabara zote zinazojengwa nchini kwa lengo la kuboresha kiwango cha elimu na hasa katika shule za sekondari za kata ambazo zilikuwa hazina maabara.
Akiongea na wanachi mjini Bukoba naibu wa waziri wa elimu tamisemi kasim majaliwa ambae alikuwa mgeni rasimi katika harambee ya kuchangisha pesa zitakazo tumika katika ujenzi wa maabara amesema zoezi la ujenzi wa maabara katika shule za sekondari si la wananchi pekee ambapo ameongeza kuwa serikali imetenga bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni moja ambazo zitatumika kununua vifaa vya maabara zote zinazojengwa nchini nakwamba zoezi la ujenzi wa maabara limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wafedha ambapo amewataka wadau wa elimu na taasisi mbalimbali zenye uzalendo na taifa hili basi wajitokeze ili kuchangia ujenzi wa maabara kwaajili ya kukuza kiwango cha elimu hapa nchini. 
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba Adoh Mapunda amesema wananchi wa manispaa ya Bukoba wamejitahidi kwa kiasi kikubwa katika kuchangia michango mbalimbali kwaajili ya ujenzi huo lakini pamoja na michango ya wananchi  halimashauri ya manispaa hiyo imelazimika kufanya halambee hiyo  kwaajili ya kuchangisha fedha kutoka kwa wadau mbalimbali wa elimu kwalengo la kukamilisha zoezi hilo la ujenzi wa maabara kwaajili ya kutekeleza agizo la rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete.
Nao baadhi ya wadu mbalimbali waelimu waliojitokeza katika harambee hiyo wamezitaka halmashauri nyingine nchini kuiga na kufuata mfano uliotumiwa na halmashauri ya manispaa ya Bukoba kwa kuanzisha harambee ambayo imefanikisha kupatikana kwa pesa tasilimi zaidi shilingi miloni arobaini na nne hali ambayo sasa inaleta matumaini ya kukamilisha ujenzi wa maabara katika shule zote za sekondarai zilizopo katika manispaa hiyo.

Post a Comment

 
Top