0

Chid Benz akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar.

HATIMAYE  msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rashid Makwiro 'Chid Benz' leo asubuhi amepata dhamana baada ya kutimiza masharti ya kesi yake ya kukamatwa na dawa za kulevya.
Msanii huyo, jana alipandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashitaka matatu ya kukutwa 


na madawa ya kulevya ambapo alishindwa kutimiza masharti ya dhamana ya shilingi milioni 1 pamoja na wadhamini wawili wasiokuwa na hatia.

Kesi yake itasikilizwa tena Novemba 11 mwaka huu.

Post a Comment

 
Top