0
 Simba akiwa ameuwawa leo na kuletwa kijijini katika ofisi ya kijiji cha Namihu kilichopo kata ya Mbaya wilayani Liwale mkoani Lindi
 Wananchi wa kijiji cha Namihu na vijiji jirani waliofika katika kijiji hicho kumwangalia simba aliyeuwawa
 Wananchi wa kijiji cha Namihu na vijiji jirani waliofika katika kijiji hicho kumwangalia simba aliyeuwawa


 Wananchi wa kijiji cha Namihu na vijiji jirani waliofika katika kijiji hicho kumwangalia simba aliyeuwawa
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Namihu wanashindwa kuhudhulia masoma baada ya kijiji hicho kuvamiwa na Simba na kandokando ya shule kuna zizi la kuku walivamia simba na kuweza kula 10 wa bwana Salehe Kapunju.

Na Mwandae Mchungulike,Anna Millanzi na Briligita Kambona,Liwale

Wakazi wa kijiji cha namihu wilayani Liwale mkoani Lindi wakumbwa na Taharuki mara baada ya kijiji chao kuvamiwa na simba.

Akizungumza na wandishi wa habari mtendaji wa kijiji hicho leo bwana Amidu  Mwembe amesema ni takriban siku sita sasa tokea simba hao wavamie katika kijiji hicho .

Aidha mtendaji huyo alisema taarifa ya kuwepo kwa wanyama hao katika kijiji cha Namihu alizifikisha mapema wilayani lakini askari hao walifika baada ya siku ya tatu ndipo walipofanikiwa kumuua simba mmoja huku wengine wakikimbilia katika maeneo ya msituni  kijijini hapo. 

Kwa upande wa waathirika wa kijiji hicho bwana Haji Mchunga na  Salehe Kapunju  walisema simba hao wamefanya uharibifu kwa kula mifugo yao ya kuku jumla ya  30 na wameomba msaada wa kuwawezesha kwakuwa mifugo yao ilikuwa ndio tegemeo lao pia wakiilaumu serikali kwa kuwanyang’anya wananchi waishio jirani na mbuga siraha ambazo zingeweza kuwalinda na wanyama wakali kama hao.

Huku Salima Kijoga akiongea kwa niaba ya kinamama alisema wanashindwa kutekeleza majukumu yao kama vile kwenda shamba kulinda mazao yao yanayoliwa na wanyama waharibifu.

“Katika kata ya Mbaya kuna tatizo kubwa la chakula kutokana na tatizo la Simba na wanafunzi wanashindwa kwenda shuleni na leo wakithamini sana wanyama kuliko binadamu sio vizuri kwani sisi binadamu tunathamani kuliko wanyama”alisema Salima.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Namihu Emanueli Mdidi alisema hata idadi ya mahudhulio ya wanafunzi imepungua kwa kushindwa kufika shuleni kwa kuhofia wanyama hao.

Diwani wa kata ya Mbaya bwana Ali Kioi amekili tatizo la kuchelewa kwa askari wa wanyamapori ni ukosefu wa usafiri na aliongeza kusema tatizo la kuvamia wanyama katika kijiji cha Namihu halijawahi kutokea takribani miaka 15.

Post a Comment

 
Top