0
Fousseni Diabate kutoka MaliHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionFousseni Diabate
Leicester imemsajili mshambuliaji wa Mali Fousseni Diabate kutoka klabu ya ligi ya daraja la pili nchini Ufaransa Gazelec Ajaccio kwa dau lisilojulikana.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 ametia saini kandarasi ya miaka minne na nusu na klabu hiyo ya Uingereza.
Akiwa kinda wa chuo cha soka cha Stade Rennais , anaweza kucheza kama winga ama hata mshambuliaji na ameichezea klabu yake mara 20.
Diabate ameiwakilisha Mali katika soka ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 na 23.

Post a Comment

 
Top