0
Mji mkuu wa Qatar, DohaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMji mkuu wa Qatar, Doha
Saudi Arabia, Misri, Bahrain na milki ya nchi za kiarabu wamekata uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar wakiilamaua wa kuvurufa ene hilo.
Nchi hizo zimeilaumu Qatar kwa kuunga mkono ugaidi likiwemo kunduoi la Muslim Brotherhood.
Shirika moja nchini Saudi Arabia linasema kwa limefunga mipaka yake na kusitisha usafiri wa ardhini, baharini na angani.
Lilinukuu maafisa wakisema kuwa hatua hiyo ni ya kulinda usalama wa nchi kutokana na hatari za ugaidi na itikadi kali.
Misri nayo imefunga anga zake na bandari kwa Qatar, kwa mujibu wa wizara ya mashauri ya nchi kigeni.,
Milki ya nchi za kiarabu imewapa wanadiplomasia wa Qatar saa 48 kuondoka nchini humo.
Abu Dhabi inaishutumu Qatar kwa kufadhili ugaidi na itikadi kali.
Shirila la taifa la habari nchini Bahrain nalo limesema kuwa nchi hiyo inataka uhusiano na Qatar kwa kuvuruga usalama wake na kuingilia ndani masuala yake ya ndani.

Post a Comment

 
Top