0
Pamoja akiwa mwenye umri mdogo wa miaka 8, Hugh Herr alikuwa mwenye shauku na ndoto kubwa ya kuwa mkwea milima (Rock Climber), na aliweza kufanya hivyo kwa wakati huo baada ya kuanza kupanda mlima uliopo nchini canada wenye urefu unaofikia 3,544 (11,67ft) unaojulikana kwa jina la Mount Temple. Alipofikia umri wa miaka 17 ikiwa ni mwezi januari 1982 Herr aliendelea kupigania kufanikisha ndoto yake kwa kupanda mlima mwingine uitwao Mount Washington uliopo mji wa New Hampshire nchini mwake Marekani.
Kwa wakati huu akiwa na rafiki yake wa karibu Jeff Blatzer aliyekuwa na umri wa miaka 20 waliweza kuanza safari yao ya kuamua kupanda mlima Washington, huku kukiwa ni kipindi cha baridi na barafu kali iliyokuwa kwenye kiwango cha -29 C. Hali hii kwao haikuwa kikwazo cha kuwazuia kutimiza ndoto yao waliyokuwa nayo kwa muda mrefu tangu hapo awali. Muda mchache baada ya kupanda mlima ule wakiwa katika kutimiza ndoto yao ghafla wakaanza kuteseka kutokana na hali ile ya baridi na barafu kali iliyowazidi na ikawa ni changamoto kubwa kwao kuendelea kukwea katika mlima ule; ndipo wote wawili walipochoka wakaamua wajiachie na kuangukia katika bonde lililokuwa chini yao.
“Commitment leads to action. Action brings your dream closer.”
-Marcia Wieder
Baada ya tukio hilo la kuanguka kwa Herr na rafiki yake, kwa pamoja walijikuta kwenye hali ngumu baada ya kuchukua muda wa siku 4 kabla ya kuokolewa wakiwa katika hali ya kuzidiwa na baridi kali iliyofanya watengeneze pango dogo kwa kupitia barafu na kuamua kukumbatina pamoja ili kuamsha hali ya joto la kuwasaidia dhidi ya hali ile ya baridi. Walipofanikiwa kuokolewa na baada ya miezi miwili kupita ikiwa ni mwezi March, Herr alijikuta akipoteza miguu yake yote miwili baada ya madaktari kugundua haiwezekani kupona kutokana na kuumia sana na kuamua kuikata kutokana na ajali aliyoipata. Lakini kwa upande wa rafiki yake ambaye ni Jeff, yeye alijikuta akipoteza vidole vya mguu wa kushoto na mkono wa kulia.
Hapo ndipo Herr alijikuta akipewa agizo kutoka kwa madaktari zake la kuacha mara moja suala la kukwea milima baada ya kupoteza miguu yake yote miwili, lakini jambo hilo lilikuwa gumu kwa Herr kuacha kufanya kwa kuwa ndani yake alipenda kuwa mkwea milima atakayeweka rekodi katika taifa lake. Na ndivyo ilivyokuwa na alifanikiwa katika hilo, kwani leo hii Herr anatajwa kama mtu bora zaidi (the best) aliyeweza kukwea milima katika kipindi kigumu ikiwa hadi leo hii pamoja na kutokuwa na miguu yake yote miwili.
Ninaweza kusema mambo mengi kuhusu mtu huyu ambaye hadi sasa kwa mahali alipofikia ni pakubwa sana, ila kwa machache haya tunaweza kujifunza jambo kubwa sana kwetu. Kwa sasa pia Herr ni mmiliki wa kampuni ya kiteknolojia (Center For Extreme Bionics) inahusika na kutengeneza vifaa vya bandia vya kuwekeza kwenye miili ya watu waliopoteza viungo vyao vya asili kama vile mikono, miguu, nakadhalika, akijulikana kama Dr. Hugh Herr, hii ni baada ya kufanikiwa kujiendeleza katika chuo kikuu cha Harvad nchini Marekani.
Unaweza kufikiri binafsi juu ya mtu huyu jinsi gani alivyokuwa na shauku kubwa juu ya kutimiza ndoto yake? Mara nyingi sana ni ngumu kwa watu wengi kufikia hatua ya kiwango cha juu cha kujitoa ili kutimiza ndoto zetu. Herr hakuweza kukata tamaa hata baada ya kupoteza miguu yake, na unaona wazi kabisa hakupoteza miguu yake kwa ajili ya jambo lingine lolote bali ni kwa ajili ya safari ya kutimiza ndoto yake aliyokuwa nayo muda mrefu, na pamoja na kupoteza miguu yake hiyo haikumfanya arudi nyuma na kuacha kuifuata ndoto yake kwa mara nyingine. Alikuwa radhi kufanya vizuri zaidi pamoja hakuwa na miguu yake halisi akitumia miguu ya bandia (prosthetic legs), na aliweza kufanya vyema zaidi kuliko mwanzo alivyokuwa na miguu yake.
Kuna sababu nyingi sana nyuma ya mtu yoyote anayetaka kukata tamaa kwenye jambo fulani. Unaweza kukata tamaa kwenye mahusiano, kwenye elimu, kwenye kazi au biashara unayoifanya; fahamu kuna kitu kinachotupelekea kukata tamaa binafsi. Nakushauri ni vyema ufahamu ni nini kinachotaka kukupelekea kukata tamaa kwenye ndoto yako, usikubali kukata tamaa haraka kwa sababu ya kushindwa mara moja juu ya jambo fulani bali unahitaji kupambana hadi mwisho ili kuhakikisha unafikia ndoto yako. Kumbuka wakati umelala usiku kwa amani na furaha kwenye kitandani chako, kuna wengine wanazurura mitaani wakiwa hawana mahali pa kwenda na kulala kama wewe. Lakini watu hawa hawakati tamaa kwenye maisha yao na wanazidi kusonga mbele kila kukicha. Ni vigumu sana kwetu kufikiri watu hawa wana uwezo gani wa kupambana na maisha yao kila panapokucha pasipo kukata tamaa.
Kuna kipindi fulani unapokuwa na shauku na ndoto fulani unayotaka ifanikiwe katika maisha yako, itakubidi ujitoe kikamilifu pasipo kuangalia gharama ya aina yoyote iliyopo mbele yako inayotaka kukuzuia kufanya hivyo, ilimradi kuhakikisha unatimiza na kuifikia ndoto yako uliyonayo. Nakusihi usitazame mazingira ya aina yoyote ile yanayokuzunguka bali amua kuweka msimamo wa kusonga mbele ili uweze kuhakikisha unafikia ndoto yako na kufanikiwa katika maisha yako. Haijalishi ni hatari gani inayojitokeza mbele yako kukuzuia kutimiza ndoto yako, songa mbele hadi uone matokeo makubwa kwenye hiyo ndoto ili uweze kubadili maisha yako kuwa kwenye viwango (level) nyingine. Usijaribu kujihurumia dhidi ya vikwazo vinavyojitokeza mbele yako hata kuacha kutimiza ndoto yako uliyonayo, kujihurumia ni kuamua kupoteza nafasi ya ushindi maishani mwako.
“Does anyone think that victory is possible without facing danger?”
-Franklin D. Roosevelt
Jiulize ni nini ndoto ya maisha yangu? Je, umekata tamaa kufuata na kuishi ndoto yako? Ni jambo gani linalokuzuia muda huu kuitimiza ndoto uliyonayo? Kama Herr hakukata tamaa kuifata ndoto yake hadi kufikia kupoteza miguu, ni kwa nini wewe uwe miongoni mwa watu wanaokata tamaa muda huu mapema kwa ajili ya kutimiza ndoto waliyonayo. Nakusihi inuka na amua kutimiza ndoto yako kwa faida yako na ya kizazi chako hapo badae.
Kila unapotaka kukata tamaa, jiulize ni kwa nini unataka kukata tamaa? (Why you give up?) Kisha mkumbuke Hugh Herr. Kumbuka ni wewe unayetakiwa kupambana kwa ajili ya kuhakikisha unatimiza ndoto yako, matarajio yako, malengo na mipango uliyonayo, nakadhalika. Kama ukikata tamaa leo, amini kabisa hutoweza kufikia mahali popote unapotaka kufika katika maisha yako.
JIAMINI NA AMINI UNAWEZA. ISHINDOTOYAKO.
Be Unstoppable! Don’t Stop. Never Give Up On Your Dream.
hugh-herr-1

Post a Comment

 
Top